• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA

Posted on: March 28th, 2025

RC MTANDA AFUNGA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Machi 28, 2025 amefunga mafunzo ya ufugaji wa samaki kwa njia ya Vizimba na kutoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo ya siku 15 kwenye chuo cha wakala wa Elimu ya Uvuvi Feta, Nyagezi wilayani Nyamagana, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa hakuna sababu za vijana kukaa vijiweni wakati zipo fursa mbalimbali za kuwainua kiuchumi.

Amesema Serikali ya awamu ya sita kwa kutambua nguvu kazi ya vijana imetoa fedha nyingi katika mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ambao umekuwa na tija katika awamu hii ya kwanza.

"Jumla ya boti 160 za kisasa za uvuvi zimetolewa kwa wanufaika 3, 295 na vizimba 222 kwa wanufaika 1,214 na mikopo hiyo imetolewa bila riba na benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania TADB", Mhe. Mtanda

Aidha amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuja na mageuzi chanya baada ya kupata mafunzo hayo hasa kuongeza Uzalishaji wa samaki ambao takwimu zinaonesha bado upo chini kutokana na sababu mbalimbali ukiwemo uvuvi haramu na tabia nchi.

Mhe.Mtanda ameipongeza pia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuandaa mafunzo hayo yenye lengo la ukuzaji viumbe maji na pia kukuza biashara kupitia rasilimali hizo.

Ameongeza kuwa bado ulaji wa samaki kwa  mtanzania kwa mwaka upo chini ambao ni kilo 7-8 wakati inatakiwa ulaji uwe kilo 20,hivyo mafunzo hayo yatakuwa ni muarobaini wa changamoto hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa Kampasi ya Mwanza kutoka chuo cha wakala wa Elimu ya Uvuvi FETA Bw.Steven Lukanga amesema kwa siku 15 washiriki hao wamejifunza ukuzaji wa samaki kibiashara na masoko yake,kuhakiki ubora wa maji,afya na magonjwa ya samaki,mfumo wa ukuzaji wa samaki na utengenezaji wa vyakula na Uzalishaji samaki kwenye vizimba.

"Tunaishukuru Serikali kwa kuendelea kuiinua na kuiboresha sekta ya Uvuvi hapa nchini,ombi letu kama chuo itambuliwe mipaka kati ya wavuvi wa asili na wenye vizimba kutokana na kuibuka kwa migogoro ya mara kwa mara",Makanga.

Jumla ya washiriki 172 ambao ni wafugaji samaki na Maafisa Uvuvi kutoka mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na Dar-e-s-Salaam,Lindi,Morogoro na Pwani wamepata mafunzo hayo na kutunukiwa vyeti.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.