• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AFUNGA RASMI MICHEZO YA SHIMISHEMITA MWANZA

Posted on: September 5th, 2024

RC MTANDA AFUNGA RASMI MICHEZO YA SHIMISHEMITA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda akimuwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo Septemba 5, 2024 amefunga rasmi Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) kwenye uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Akizungumza na wanamichezo hao Mhe. Mtanda amesema Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuinua sekta ya michezo, sanaa na utamaduni na ni muhimu kwa watumishi wa Serikali kumuunga mkono mchezaji namba moja nchini ambaye ni Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kushiriki katika michezo hiyo iliyoandaliwa kwa ajili yao.

"Michezo mahala pa kazi inawajengea ari ya kuchapa kazi kwani ukamilifu wa afya inawajengea uwezo mkubwa wa kufanya kazi tena kwa weledi, huku mkiwaa mmeimarika wakati wote lakini pia ina wajengea uzalendo." RC Mtanda.

Aidha, amewataka wanamichezo hao kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za michezo ili malengo ya shirikisho hilo yatimie na ametumia jukwaa hilo kuzionya Halmashauri zilizokiuka taratibu na kupelekea kuondolewa kwenye michezo hiyo kuhakikisha hawafanyi hivyo tena kwani kuwapelekea watumishi kuwakosesha haki yao ya kujumuika na wenzao katika michezo.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda piaa amewapongeza wanamichezo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Wilaya ya Kwimba kwa Mkoa wa Mwanza kwa kushika nafasi za tatu kwenye baadhi ya michezo.

Awali, Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo Henry Kapela alibainisha kuwa jumla ya wanamichezo 2160 kutoka kwenye Halmashauri 100 wameshiriki mwaka huu tofauti na 45 za mwaka jana na kwamba uhamasishaji na maandalizi ya michezo ya mwakani unapaswa kuanza sasa.

Vilevile, ametoa rai kwa uongozi wa mashirikisho hayo ngazi ya Halmashauri kuzingatia taratibu na sheria za michezo chini ya shirikisho hilo ili kuwaepusha na usumbufu wa kuondolewa kama ilivyotokea kwa halmashauri 3 ambazo ni Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Dodoma na Manispaa ya Moshi.

Mshindi wa jumla wa michezo ya SHIMISEMITA kwa mwaka huu ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambao wamekua wa kwanza kwa michezo 9. Aidha  michezo hiyo kwa mwaka huu imechagizwa na kaulimbiu isemayo "Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Taifa Endelevu".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.