• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA GoTHOMIS NA LISHE

Posted on: March 12th, 2025

RC MTANDA AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA GoTHOMIS NA LISHE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amefungua kikao cha kamati ya afya ya msingi mkoani humo na kuhimiza utekelezaji wa mfumo wa taarifa za usimamizi wa uendeshaji wa afya wa Serikali ya Tanzania katika vituo vya huduma za afya(GoTHOMIS) na afua za Lishe lengo likiwa Mkoa huo uwe kinara Kitaifa katika utoaji bora wa huduma hizo.

Akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo leo Machi 12, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, Mtanda ametoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha mfumo huo unafungwa kwenye vituo vyote vya afya na apatiwe taarifa ya maendeleo yake kabla na baada ya matumizi hayo.

Amesema kwa mujibu wa takwimu Mkoa wa Mwanza unashika nafasi ya 3 kitaifa kwa utekelezaji wa huduma ya GoTHOMIS, amehimiza kazi ya ziada iendelee kufanyika ili tushike nafasi ya kwanza.

"Serikali inaendelea kuwekeza katika miradi ya afya, lakini hatuna budi kuhakikisha yanakuwepo makusanyo sahihi ya fedha ili zisaidie kuboresha huduma hiyo na nyinginezo", Mkuu wa Mkoa.

Kuhusu afua za Lishe, Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha maafisa lishe kutoka halmashauri zote mkoani humo kuhakikisha wanafanya vizuri ili kuepukana na hali ya udumavu na ukosefu wa afya kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

"Hapa Afisa Lishe Mkoa ametupitisha katika taarifa yake bado Halmashauri nyingi hazifanyi vizuri,na hili ni agizo la Mhe.Rais kwa sisi wakuu wa mikoa kulisimamia vizuri zoezi hili,sasa sitakuwa tayari kuona baadhi ya maafisa lishe mkifanya uzembe,"amesisitiza Mtanda wakati akifunga kikao hicho.

Wakati huo huo, Waziri wa Afya Mhe. Jenister Mhagama amepata wasaa wa kuwasalimu wajumbe wa kikao hicho alipofika Ofisi ya mkuu wa mkoa akielekea katika majukumu mengine na kusisitiza bado magonjwa yasiyoambukiza ni changamoto na kutoa rai kubadili mtindo wa maisha ukiwemo ulaji na kufanya mazoezi.

Kikao cha kamati ya afya ya msingi ya Mkoa kimewajumuisha wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri, waganga wakuu wa wilaya,maafisa lishe pamoja na viongozi wa dini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.