• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKARIBISHA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MICHEZO

Posted on: September 6th, 2024

RC MTANDA AKARIBISHA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MICHEZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh.Said Mtanda leo Septemba 6,2024 amekutana na wataalamu wa michezo kutoka nchini Brazil na katika mazungumzo nao amewaalika kuwekeza katika michezo hasa kutokana na Mkoa huo kuwa na hazina ya vipaji.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ofisi kwake na wataalamu hao wa soka,Mtanda amebainisha licha ya kuwa na vijana wenye vipaji lakini tunakwama namna ya kuviendeleza hivyo bado tunahitaji nchi kama Brazil iliyopiga hatua kubwa katika sekta hiyo.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mkereketwa wa mchezo wa soka amewaambia wataalamu hao kuwa watanzania wana imani kubwa na Taifa la Brazil katika mchezo wa soka hasa kutokana na hatua kubwa waliyopiga na vipaji walivyonavyo

Ameongeza kuwa  michezo kwa sasa ulimwenguni ndiyo nguzo imara ya ajira, lakini kabla ya mchezaji huyo kupata soko ni lazima apitie misingi muhimu ambayo hapa kwetu bado wanaikosa.

"Ili mchezaji uwe wa Kimataifa ni lazima uwe na nidhamu,upitie timu za Taifa za vijana,na misingi mingine madhubuti kutoka shule maalum za michezo," amefafanua Mtanda wakati akitoa taarifa fupi kwa vyombo vya habari mara baada ya mazungumzo na wageni wake.

Kiongozi wa msafara huo ambaye pia amemwakilisha  Balozi wa Tanzania nchini Brazil,Beatus Kalumuna amesema lengo la ziara hiyo kwanza ni kuimarisha uhusiano wa Diplomasia ya michezo baina ya Tanzania na Brazil na kubadilishana uzoefu wa kitaalamu pia kupitia sekta hiyo.

"Hapa wamekuja wataalamu tofauti wakiwemo wa kuibua vipaji,wa kuviendeleza,mwakilishi kutoka Cruzelo shule ya soka ya mchezaji Ronaldo Nazari de Lima na mtaalamu wa michezo ya Olympiki,"Kalumuna

Wakiwa mkoani Mwanza watashuhudia baadhi ya michezo ya soka chini ya miaka 21 pamoja na fainali ya Ndondo Cup na kutoa ushauri wa kitaalamu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.