• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AMSHUKURU DKT. SAMIA KUANZISHA OFISI YA KANDA YA ZIWA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA

Posted on: June 30th, 2024

RC MTANDA AMSHUKURU DKT. SAMIA KUANZISHA OFISI YA KANDA YA ZIWA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha Ofisi ya kanda ya ziwa ya mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya na kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini.

Shukrani hizo amezitoa leo wakati alipokua akitoa salamu katika kilele cha maadhimisho ya Kitaifa ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani, maadhimisho yaliyofanyika leo Juni 30 2024, kwenye uwanja wa Nyamagana

Akitoa taarifa ya hali ya dawa za kulevya katika Mkoa wa Mwanza kuanzia mwaka 2018 hadi 2023, Mhe. Mtanda amesema jumla ya wananchi waliopatikana na dawa za kulevya aina ya bangi ni 1797, mirungi 294, dawa za kulevya (cocaine, heroine na nyingine) 51 na kufanya jumla ya dawa zote kuwa 2142.

"Takwimu hizi zinabainisha kwamba bishara na matumizi ya dawa za kulevya hapa Mkoani Mwanza ni kubwa na inahitaji msukumo mkubwa kutoka kwa Serikali pamoja na wadau mbalimbali ili kuendelea kupambana na wazalishaji, wasambaji na watumiaji wa dawa za kulevya".

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kutokukubali matumizi ya dawa za kulevya kwani zinaharibu jamii, na kama tutashirikiana pamoja tunaweza kulikabili janga hili.

Kadhalika Mhe. Mtanda amesema Mkoa huo unaendelea kusimamia na kufuatilia kwa karibu miradi ya kimkakati na miradi yote inayoendelea kujengwa ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha (Value for Money).

Maadhimisho ya Kitaifa ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani yamehitimishwa leo Mkaoni Mwanza na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama cha Mapinduzi, Viongozi wa kimila, mashirika mbalimbali, wadau na wananchi huku mgeni rasmi akiwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Kassim Majaliwa (Mb.).

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.