• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA APIGA GIA ANGANI ATANGAZA MOTISHA PAMBA JIJI IKISHIKA NAFASI ZA JUU LIGI KUU

Posted on: February 15th, 2025

RC MTANDA APIGA GIA ANGANI ATANGAZA MOTISHA PAMBA JIJI IKISHIKA NAFASI ZA JUU LIGI KUU


Timu ya soka ya Pamba Jiji FC ambayo mzunguko wa lala salama ya ligi kuu imeingia na gia kubwa kwa kutoa dozi za ushindi kwa timu pinzani, sasa imetangaziwa dau nono endapo itamaliza ligi hiyo huku ikiwa imeshika nafasi za juu kuanzia ya tano hadi kumi.

Akizungumza na wachezaji wa Pamba Jiji mapema leo Ofisini kwake kabla ya timu hiyo kushuka dimbani kumenyana na Wagosi wa Kaya (Coastal Union), Mtanda amesema awali malengo yalikuwa msimu huu ni kuhakikisha wanabaki ligi kuu.


Ameongea kuwa, kutokana na mwendo mzuri walionao malengo ni kushika nafasi za juu na hilo linawezekana endapo watashinda mchezo dhidi ya Coastal Union na Mashujaa FC.

"Mkakati wa kupigania kubaki ligi kuu huo sasa tunaugeuzia kisogo, tuanze kupigania nafasi za juu na motisha nono itakuwepo tukishika nafasi ya tano au kumi,"amesisitiza Mtanda ambaye pia ni mlezi wa Pamba Jiji.


Amewakumbusha wachezaji hao kuongeza bidii kwa kila mchezo wao kwani lala salama ya ligi kuu ni ngumu na waepuke aina yoyote ya utovu wa nidhamu ambao utaigharimu timu.

"Epukeni kufanya madhambi dimbani na kupewa umeme (akimaanisha kadi nyukendu) hii itasabisha mzigo kwa timu kwa kumkosa mchezaji muhimu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Katika mazungumzo hayo Mtanda amewakabudhi wachezaji hao Tshs. milioni 11 mchango aliopewa na wadau wa soka walioamua kumchangia na kubaki milioni 4 ili zikamilike milioni 15 ahadi aliyowapa wachezaji hao ya shs milioni 30 baada ya ushindi wao dhidi ya Azam FC,awali aliwakabidhi milioni 15.

Katika mpambano wake wa leo uliopigwa dimbani CCM Kirumba Wana TP Lindanda wamezidi kuwasha endiketa kuelekea nafasi za juu katika msimamo wa ligi kuu baada ya kuwachezesha ngoma ya Mdumange timu ya Coastal Union kutoka Tanga kwa kuwabugiza mabao 2-0.

Kwa ushindi huo timu hiyo sasa imekwaa hadi nafasi ya 8 na mtaji wa pointing 21 kibindoni huku ikijiandaa na safari ya Kigoma kuwafuata Mashujaa FC  mchezo utakaopigwa siku ya Jumatano Februari 19 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.