• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ASHIRIKI HAFLA YA UVISHAJI NISHANI MAAFISA, WAKAGUZI NA ASKARI POLISI

Posted on: May 24th, 2024

RC MTANDA ASHIRIKI HAFLA YA UVISHAJI NISHANI MAAFISA, WAKAGUZI NA ASKARI POLISI


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura leo  24 Mei, 2024 amewavisha nishani Maafisa, Wakaguzi, na Askari wa vyeo mbalimbali kutoka Mikoa ya Kanda ya ziwa kwenye Viwanja vya FFU Jijini Mwanza.

Akizungumza kwenye hafla hiyo IGP amewataka Jeshi la polisi kusimamia maelekezo ya kijinai kwani ndio dira ya utendaji kazi wa jeshi hilo na akawataka kusimamia utendaji kazi kuanzia ngazi za chini.

"Tutengeneze madawati ya ufuatiliaji na tathmini ya maelekezo kuanzia ngazi za juu hadi chini kwa ajili ya kuleta uelewa kwa askari mmoja mmoja kwani italeta urahisi kuratibu na kusimamia." IGP Wambura.

Aidha, amemshukuru Rais Samia kwa kuruhusu uvishaji nishani lakini pia upandishaji wa Madaraja kwa maafisa na askari wa jeshi hilo kwani kwa muda mrefu walikosa fursa na ujenzi wa makazi ya Askari na Maafisa na ameonesha kufurahishwa na maendeleo hayo huku akitamani jeshi hilo kuwa la mfano duniani.

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa pongezi kwa jeshi hilo kwa kuimarisha amani nchini kwa kusimamia weledi kwenye kazi hasa nidhamu inayosaidia utulivu wa raia.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kushirikiana na jeshi hilo na majeshi mengine nchini kuimarisha usalama kwenye makazi yao kwani Jeshi hilo limejitoa kuhakikisha wanawalinda raia na mali zao ili wawe huru kufanya shughuli za kujiletea maendeleo.

"Hongereni sana kwa kuvishwa nishani, nataka niwaambie kuwa taasisi yotote ni lazima isimamie haki, ijiepushe na matendo ya kuharibu maadili na haki kwa jamii, askari wote nataka mjenge heshma yenu wenyewe na ya jeshi letu makini." RC Mtanda.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa ametumia wasaa huo kuwapongeza wote waliovishwa nishani na ameishukuru Ofisi ya Mkoa wa Mwanza kwa ushirikiano wanaolipatia jeshi hilo kila wakati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.