• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATAKA ADHABU KWA WANAFUNZI IZINGATIE MIONGOZO YA ELIMU

Posted on: September 20th, 2024

RC MTANDA ATAKA ADHABU KWA WANAFUNZI IZINGATIE MIONGOZO YA ELIMU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Walimu Mkoani humo kutoa adhabu kwa wanafunzi kulingana na miongozo na sheria za nchi ili kujenga tabia ya ushirikiano na umoja baina ya wazazi na walimu.

Amesema hayo leo ijumaa tarehe 20 Septemba 2024 wakati akizungumza na wazazi na wanafunzi wa shule za Blessing modal wakati wa mahafali ya wanafunzi wa darasa la saba na awali.

Aidha, ameupongeza uongozi na walimu wa shule hiyo kwa mafanikio wanayoyapata mwaka hadi mwaka mpaka kufikia hatua ya kufaulisha kwa daraja A kwenye masomo na kupelekea wazazi kuwapeleka watoto wao hata kuzidi elfu moja tofauti na wanafunzi 8 tu wakati inaanzishwa.

Vilevile, amewapongeza kwa kulinda tamaduni, miiko, desturi, silka na mila za kitanzania na kuwalea watoto kwenye maadili safi kwa kuwakuza kwenye miongozo ya kidini bila ubaguzi wala upendeleo wa upande mmoja.

"Nimefurahishwa sana na onesho lililofanywa hapa na nimeamini hapa hata kama shule haina dini lakini mnazingatia imani za wanafunzi wenu, na mnawafundisha hata kupika nimependezwa sana". Amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Akizungumzia maadili, Mhe. Mtanda amewataka wazazi kushirikiana na walimu wanaowalea watoto wakati wawapo shuleni na kuwa na mawasiliano ya karibu na shule ili kusimamia kwa pamoja makuzi ya watoto.

"Msiwaache watoto wakajilea wenyewe au kwa msaada wa wafanyakazi, mtapoteza upendo kwa watoto wenu hakikisheni mnatenga muda kwa watoto ili mtengeneze mapenzi na watoto wenu".

Vilevile, ametumia jukwaa hilo kutoa wito kwa jamii kulinda amani nchini ili wananchi waendelee kuwa na utulivu wakati wanaendelea na majukumu yao ya kujipatia kipato hususani kwenye kilimo, uvuvi, uchimbaji wa madini na biashara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.