• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA MUDA WA MIEZI MITATU WANAODAIWA 5% YA MIKOPO YA HALMASHAURI KUZIREJESHA

Posted on: June 28th, 2024

RC MTANDA ATOA MUDA WA MIEZI MITATU WANAODAIWA 5% YA MIKOPO YA HALMASHAURI KUZIREJESHA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wanachi wote wanaodaiwa marejesho ya mikopo waliyochukua kutoka Halmashauri ya wilaya ya Magu zaidi ya mil. 148 kuhakikisha wanazirejesha fedha hizo ndani ya miezi mitatu ili na wananchi wengine wenye sifa na vigezo waweze kunufaika.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo mapema leo Juni 28, 2024 alipokuwa akizungumza katika kikao cha Baraza Maalumu la Madiwani cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) za mwaka 2022/2023 na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa kupata hati inayoridhisha na ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

"Mkopo huu sio hisani na wala sio mgao wa kula, wale wote waliopitiliza muda wa marejesho watafutwe wabanwe wazilipe ili tuweze kuwakopesha wanawake wengine, nchi hii ina wahitaji wengi".Mtanda

Mkuu huyo wa Mkoa amesema nia ya Serikali kutoa 5% ya fedha ya mapato ya ndani za  Halmashauri ni kuwasaidia wanawake katika harakati za kupambana na kujikomboa na umaskini kwa kuwawezesha kutumia fedha hizo katika kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha Mhe. Mtanda ameitaka Halmashauri hiyo kuhakikisha wanamaliza hoja 11 zilizobakia kwa wakati na kusema kuwa ameridhishwa na namna walivyojipanga kuzimaliza hoja hizo. Kadhalika amewataka kuwasilisha Mkoani mpango kazi wa namna ya kuzimaliza hoja hizo ifikapo tmJunu 29,2024 mwaka huu ili mpango kazi huo uunganishwe na utumwe Wizarani TAMISEMI.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mhe. Simon Pandarume amesema wao kama Halmashauri wana ushirikiano wa kutosha kwani wamefanikiwa kuongeza mapato ya ndani kutoka sh. bil. 2.4 na kufikia bil. 4.4 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

"Tumefungua Shule nyingi kwa mapato ya ndani, 19 mpya za Sekondari na 7 za Msingi kwa miaka minne, tumepeleka pia fedha nyingi kwenye zahanati, nyumba za watumishi, wakiwemo waalimu". Amesema Mhe. Pandarume.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.