• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA SIKU 7 KWA WAKUSANYA USHURU MAGU KUWASILISHA FEDHA BENKI

Posted on: June 13th, 2024

RC MTANDA ATOA SIKU 7 KWA WAKUSANYA USHURU MAGU KUWASILISHA FEDHA BENKI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa muda wa Siku 7 kwa watumishi wanaokusanya mapato kwenye halmashauri ya Wilaya ya Magu kuhakikisha wanawasilisha fedha zaidi ya Tshs. Milioni 15 benki na wasipotekeleza hayo watawachukulia hatua za sheria.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo Juni 13, 2024 wakati akizungumza na baadhi ya wazee, wadau wa maendeleo pamoja na watumishi wa Halmashauri na kubaini kuwa Halmashauri hiyo imekusanya mapato ya ndani kwa 87% tu kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2024.

"Halmashauri yenu haifanyi vibaya lakini haijafikia malengo ya ukusanyaji wa wapato ya ndani, naelekeza siku chache zilizobakia halmashauri ifikishe asilimia mia na kwa wanaodaiwa zaidi ya milioni 15 ndani ya siku 7 wawasilishe benki fedha hizo." Mkuu wa Mkoa.

Mtanda amefafanua kuwa ili kutekeleza jambo hilo ni lazima kuwe na uzingatiaji wa sheria kwenye ukusanyaji pamoja na matumizi ikiwemo upelekaji wa fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo ili wananchi wapate huduma za kijamii zilizoboreshwa.

Mhe. Joshua Nathari, Mkuu wa Wilaya ya Magu amesema hawajafika lengo la makusanyo ya mapato ya ndani kwani wamekusanya Tshs. Bilioni 3.7 ambayo ni asilimia 87 ya makadirio na kwamba wameweka mkakati wa kuzifikia 92 za kisheria za OR -TAMISEMI kupitia chanzo cha Stendi ya Kisesa.

Ameongeza kuwa, kwa mwaka 2023/24 wamepokea fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za Afya, Elimu, Ardhi, kilimo, Miundombinu na kwamba nishati ya umeme imefika kwenye vijiji vyote (Gridi ya Taifa) kasoro kimoja tu na usambazaji maji inaridhisha sana.

Aidha Mhe. Mtanda amewataka wataalamu wa afya kuhakikisha wanasimamia uwepo wa madirisha ya wazee kikamilifu kwani sera ya nchi inaelekeza wazee watibiwe bure na wasitozwe chochote.

"Nataka kutoa onyo kwa wataalamu wa afya wanaowahudumia wazee na mwisho wa matibabu wanawaambia wakanunue dawa, ni marufuku kufanya hivyo kwani mnachotakiwa ni kukamilisha matibabu yao kwani Serikali inagharamia na tuweke madirisha maalumu kwa ajili yao." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.