• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA SOMO UMUHIMU WA SADAKA

Posted on: March 30th, 2025

RC MTANDA ATOA SOMO UMUHIMU WA SADAKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameikumbusha jamii umuhimu wa kutoa sadaka kwa moyo mkunjufu kwani kwa kufanya hivyo ndio maombi na sala zinaweza kupokelewa na kujibiwa kwa haraka zaidi na Mwenyezi Mungu.

Ameyasema hayo leo machi 30, 2025 alipokuwa akizungumza katika  Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Katoliki la Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Daima- Kome, Wilaya ya Sengerema Jimbo la Geita. Harambee iloyofanyika katika ukumbi wa Gold Crest Hotel, Jijini Mwanza.

"Katika changizo hili naomba tutoe kwa imani tukiamini kwamba Mungu atatusaidia kwa mambo mbalimbali kama magonjwa, migogoro ya ndoa hivyo toa kwa imani kuwa natoa sadaka hii ila Mungu maliza mgogoro wangu wa ndoa, Hivyo toa huku ukiomba”. Mhe. Mtanda

Aidha Mkuu wa Mkoa ameendelea kwa kusema unapotoa sadaka yakupasa kutoa kwa imani na sio kwa manung'uniko, amesema usitoe kwa sifa wala manung'uniko ni mambo ambayo Mungu ameyakataza.

“Na kama umegombana na ndugu yako kabla ya kutoa sadaka yako kapatane nae kwanza ili ubarikiwe. Ukitoa unapata heri na unaweka hazina yako mbinguni." - Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa pia ameitaka jamii kutoa sadaka kutokana na uwezo yaani isizidi wala isipungue kiwango ambacho mtu anakipata aidha amesema na ndio maana kuna sadaka inaitwa zaka ambayo huitajika 10% tu ya mapato na haitakiwi kupungua wala kuongezeka.

Naye Mhashamu Baba Askofu Flaviana Kassala Askofu wa Jimbo Katoliki Geita amesema harambee hiyo ya ujenzi wa kanisa Katoliki inatokana na umuhimu wa kanisa hilo na historia iliyopo ambapo mpaka sasa kanisa hilo limefikisha miaka 125, hivyo ujenzi huo unahusisha kulinda historia ya Kanisa na kisiwa cha kome.

“Ujenzi wa kanisa hili si kwa ajili ya Kanisa tu bali imebeba historia yetu kama Taifa, ambapo hapo awali miaka ya 1900 ilisaidia kuimarisha mahusiano kati yetu na wageni waliotoka nchi za ulaya kuleta injili”.

Aidha Mhashamu Baba Askofu ameendelea kwa kusema kisiwa cha kome kina vivutio na matarajio mengi hivyo kusherehekea miaka hiyo 125 ni kulinda  pia tunu na historia ambayo kisiwa hicho kinabeba.

Awali Harambee hiyo ilikusudia kupatikana kwa shilingi milioni 500, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amechangia kiasi cha shilingi milioni 5, huku jumla kuu ya fedha taslimu na ahadi ni shilingi milioni 177. Aidha sherehe ya miaka 125 ya Kanisa hilo inatarajiwa kufanyika Agosti 17 mwaka huu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.