• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA WITO KWA TAASISI NCHINI KUTENGA FEDHA ZA WATUMISHI KUSHIRIKI MICHEZO

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wakuu wa taasisi na mashirika nchini kutenga fedha za michezo na kuzitumia kwa mujibu wa vifungu vya michezo ili kuimarisha afya ya watumishi.

Ametoa maagizo hayo leo tarehe 02 Septemba, 2025 wakati akifungua mafunzo na semina kwa Viongozi, makocha na madaktari wa Michezo kutoka shirikisho la michezo ya Mashirika ya umma, taasisi na makampuni binafsi Tanzania ( SHIMMUTA).

Amesema sera za nchi zinawataka wakuu wa taasisi na mashirika kutenga fedha na kutoa kwa wakati kwa washiriki wa michezo kwenda kujumuika na wengine wakati wa kalenda ya michezo katika mikoa mbalimbali wanayokutana.

Ameongeza kuwa wafanyakazi wanaoshiriki michezo wanakua na afya thabiti hawaugui ovyo na wataleta tija kwenye ofisi kwa kupata watumishi wenye afya njema wakati wote.

Vilevile, ametoa wito kwa taasisi hizo kudhamini na kuandaa mabonanza na michuano mbalimbali ya ndani ili watumishi washiriki michezo kabla ya wakati wa kukutana kwa ajili ya michezo ya SHIMMUTA.

“Mafunzo ni sehemu ya kuboresha michezo nchini, nimeambiwa hapa wapo hadi madaktari na kweli watu wote hawa wanatakiwa kupata mafunzo ya uongozi na sio tu kutoa tiba hivyo nawapongeza maana mnawapa uwezo wa kuandaa timu kikamilifu.” Amesema Mhe. Mtanda.

Akitoa risala ya wanachama, Mwenyekiti wa SHIMMUTA Ndugu Roseline Masamu amesema mafunzo kama hayo mwaka 2023 walikua 110, 2024 walikua washiriki 114 lakini mwaka 2025 wana washiriki 130, ongezeko linaloonesha kuwa wakuu wa taasisi wanatambua umuhimu wa michezo nchini.

Aidha, amebainisha kuwa semina hiyo iliyozikutanisha taasisi 59 inakwenda sambamba na maandalizi ya michezo inayoratibiwa na umoja huo ambayo inatarajia kurindima mwezi novemba ndani ya Mkoa wa Mwanza.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA MWANZA KUCHANGAMKIA DIRISHA LA UWEZESHAJI

    September 03, 2025
  • RC MTANDA AWAASA TCCIA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZINAZOHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

    September 02, 2025
  • WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

    September 02, 2025
  • MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

    September 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.