• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAHIMIZA VIJANA UMUHIMU WA KUCHAPA KAZI KATIKA KUJILETEA MAFANIKIO

Posted on: June 15th, 2024

RC MTANDA AWAHIMIZA VIJANA UMUHIMU WA KUCHAPA KAZI KATIKA KUJILETEA MAFANIKIO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka vijana Mkoani humo kuhakikisha wanafanya kazi kwa hali na mali ili waweze kufikia malengo na mafanikio waliyo jiwekea.

Akiongea leo Juni 15, 2024 wakati alipotembelea shindano la kusaka mzalendo namba moja kwa nchi yake mwenye kujua Rais Samia amefanya nini katika Mkoa wa Mwanza (Samia Challenge)  Mtanda amesema haamini katika njia nyepesi ya mafanikio, hata  ukuu wa Mkoa, siamini kutumia ukuu wangu wa Mkoa kuniondolea umaskini wangu.

"Kwa hiyo ukitaka njia rahisi kupitia ukuu wa Mkoa basi utataka kula rushwa utawaonea watu ili upate pesa ununue ghorofa, ununue gari zuri uwe na maisha mazuri mwisho wa siku hata safari hii ya ukuu wa Mkoa itakuwa safari fupi." Amesema RC Mtanda.

Aidhe, Mhe. Mtanda amewataka Vijana hao kukaa mbali na tamaa kwani sio kila kitu wanavyo vitamani wanaweza kuvipata, hali inayoweza kuwapelekea kuishia pabaya na wakashindwa kufikia mafanikio na malengo waliyojiwekea kwa sababu ya tamaa.

Akiongelea maadili, Mhe  Mtanda amewataka vijana wa kike kutokubali kutumika vibaya au kununulika kwa kuelewa na kutambua thamani yao, kwa kuweka jitihada katika mambo wanayoyafanya na Mungu atawasaidia kwa sababu kwenye nia pana njia.

"Katika jambo ambalo nikikutana na  Vijana napenda kuwausia ni umuhimu wa kujali na kutunza afya zao, hakuna maendeleo wala mafanikio bila ya afya bora, huwezi kutimiza ndoto zako za maisha kama afya haiko sawa sawa, lakini pia afya ikishayumba utatumia fedha na muda mwingi katika kushughulikia afya zetu. Ameongeza Mhe. Mtanda.

Mtanda kadhalika amewataka Vijana hao kuhakikisha wanatenga muda wa kufanya mazoezi na kujiepusha na vitu vinavyoweza kuharibu afya ikiwemo uvutaji wa sigara, bangi, ulevi na matumizi ya dawa za kulevya, ngono zembe na vitu vyote vinavyochochea uharibifu wa afya.

Akihitimisha hotuba yake Mkuu huyo wa Mkoa amewapongeza vijana hao kwa ushiriki wao, aidha amesema hapa Mwanza Serikali ya Rais Samia ipo imara chini ya uongozi wake kama Mkuu wa Mkoa na amewataka vijana hao pia kuendelea kuiunga mkono Serikali ya awamu ya sita kwa kufanya kazi kwa bidii.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.