• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWASILISHA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA HALMASHAURI KUU ILIYOSHEHENI MAZURI

Posted on: May 31st, 2024

RC MTANDA AWASILISHA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA HALMASHAURI KUU ILIYOSHEHENI MAZURI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Mei 31, 2024 amewasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha Januari 2021 hadi Disemba 2023 kwa Halmashauri kuu ya Chama hicho iliyosheheni ya kujivunia yaliyofanywa ndani ya miaka mitatu.

Mhe. Mtanda amesema pamoja utekelezaji wa miradi lukuki katika Sekta za Afya, Maji, Miundombinu na Elimu, Mkoani Mwanza Serikali imeajiri watumishi 2697 kwenye sekta mbalimbali na Bilioni 2.5 zimetumika kulipa stahiki na kwamba inaendelea kuboresha utumishi kwa kujenga ofisi na makazi hadi kutumia Bilioni 16 Mwanza.

"Katika kuboresha Elimu ya awali kwa shule za Msingi Madarasa 53 ya mfano yamejengwa ndani ya miaka mitatu na walimu wa awali wameajiriwa hadi kufikia 979 kutoka 923 waliokuwepo awali na uandikishaji wa wanafunzi umeongezeka kutoka shule 1048 hadi 1118 sawa na ongezeko la shule 70 mpya", Mhe. Mtanda.

Ameongeza kuwa pamoja na miradi kama SEQUIP, BOOST na mingine Serikali imeendelea kuboresha masuala mazima ya Elimu hadi Elimu ya Juu hususani kwa ujenzi wa miundombinu pamoja na utoaji wa mikopo ya Elimu ya juu kwani Bilioni 136 zimetolewa kwa wanafunzi zaidi ya Elfu 40.

Katika sekta ya afya amebainisha kuwa ujenzi wa zahanati umeongezeka kutoka 274 hadi 319 na kwamba 385 zimejengwa kwenye Mamlaka za Serikali za mitaa na afua za lishe zimetengwa zaidi ya Bilioni 1 kwa ajili ya kujenga jamii yenye afya na Siha njema na vifo vya wazazi mwaka vimezidi kushuka.

Kupitia RUWASA Serikali inatekeleza miradi 38 yenye thamani ya Bilioni 112 ambapo 40 ya Bilioni 24 imekamilika na Serikali imepokea seti ya mtambo wa kuchimba visima na mradi mkubwa wa Kapripoint unapanuliwa na kuongezewa nguvu na mradi wa Butimba na usambazaji ndio dira mkononi kwa sasa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Mhe. Michael Lushinge amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kufanikisha uwasilishaji wa Ilani hiyo kwani amefikia takwa la kisheria na kufanikiwa kutoka kwenye ukwamo wa uwasilishaji huo uliodumu kwa miaka mitatu.

Mhe. Lushinge amesema siku za karibuni wamekagua miradi 31 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 200 na ametumia wasaa huo kumpongeza Mtendaji Mkuu wa MWAUWASA kwa kutekeleza kwa vitendo sera ya kuwaletea wananchi maji na hakuacha kumsifu Meneja RUWASA wa Ukerewe Mhandisi Zubeda Saidi kwa kukamilisha miradi na kubakisha nilioni 320 zilizosaidia kusambaza maji kwenye Vijiji nje ya mradi.

Halikadhalika, Halmashauri hiyo imeshauri Serikali kuweka mkazo kulisemea zao la Pamba kwani ndio linategemewa kwenye uchumi wa Mwanza na wakatoa wito kwa Sekta ya Uvuvi kuzingatiwa ili ikuze pato la wafanyabishara na ili kulinda mazalia ya Samaki wamesisitiza kuandaliwa kwa mipango ya kuzuia uvuvi haramu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.