• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA AFD KUTOA BARUA YA KUTOKUWEPO NA KIPINGAMIZI KATIKA MIRADI INAYOENDELEA

Posted on: June 4th, 2024

RC MTANDA AWATAKA AFD KUTOA BARUA YA KUTOKUWEPO NA KIPINGAMIZI KATIKA MIRADI INAYOENDELEA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 04, 2024 ofisini kwake amekutana na kufanya kikao kifupi na Mkurugenzi wa Afrika Mashariki wa Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Bibi Hellen Ngarmin ambaye yupo Jijini Mwanza kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na MWAUWASA na iliyopangwa kutekelezwa.

Akizungumza katika kikao hicho RC Mtanda ametoa rai kwa AFD kutoa barua ya kuondoa vipingamizi katika mradi wa ujenzi ili kuruhusu kuendelea na hatua inayofuata kwenye mchakato wa ujenzi wa mradi wa usambazaji mabomba na ujenzi wa matenki katika upanuzi wa mradi wa maji Butimba.

Aidha Mhe. Mtanda amesema Serikali na Wananchi wa Mwanza wanatamani kuona huduma ya usambaji maji inatekelezwa katika maeneo husika na kukamilika kwa wakati ili jamii iondokane na adha ya upungufu wa maji hivyo ni wakati sasa wa kuongeza kasi kwenye taratibu za utekelezaji.

"Mradi wa Butimba ni muhimu sana kwa kuwa hapo kabla tulikuwa na mradi tegemezi wa chanzo cha kapripoint ambao haukuwa unatosheleza mahitaji hivyo kukamilika kwa mradi huu utawanufaisha watu wengi". Amesema RC Mtanda.

Mhe. Mtanda amesema pia Mwanza ni Mkoa wa Pili kwa ukubwa na ni mji wa kiuchumi hivyo uboreshaji wa sekta ya maji utapelekea watu wengi kuvutika na kufanya uwekezaji na makazi hali ambayo itapelekea uchumi wa Mwanza kukua na kuongeza muingiliano wa watu kutoka Afrika Mashariki ambao wameunganishwa na ziwa Viktoria.

Sambamba na ufadhili wa mradi wa maji wa Butimba RC Mtanda amewashukuru AFD kwa kuendelea kufadhili miradi mingine ya kimkakati kama vile ujenzi wa matundu 104 ya vyoo kwa shule za msingi, masoko na Zahanati katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.

Naye Mkurugenzi wa Afrika Mashariki wa Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Bibi Hellen Ngarmin amesema anefurahishwa na kasi ya maendeleo ya usambaji wa huduma ya maji hasa kwa wakazi wanaoishi katika milima.

Viongozi hao kutoka Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Wametembelea Soko la  Mwaloni pamoja na miradi ya maji taka na mradi wa upanuzi wa chanzo cha Maji Safi Butimba awamu ya pili (Phase II)

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.