• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA MAAFISA ELIMU ILEMELA KUONGEZA KASI UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI

Posted on: February 10th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Maafisa Elimu wa Wilaya ya Ilemela kuanzia ngazi ya wilaya, kata hadi mitaa kuhakikisha wanakamilisha kwa asilimia 100 zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza.

Agizo hilo amelitoa leo Februari 10, 2026 wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa maabara katika Shule ya Sekondari Buzuruga, ambapo amesema hali ya uandikishaji wa watoto katika Manispaa ya Ilemela bado hairidhishi ikilinganishwa na wilaya nyingine alizotembelea.

Mhe. Mtanda amesema baadhi ya wilaya tayari zimevuka lengo la uandikishaji na kufikia zaidi ya asilimia 95, hali iliyomfanya atoe wito kwa wazazi na walezi kutimiza wajibu wao kwa kuhakikisha watoto wote wenye sifa wanaandikishwa shule.

“Ninamuagiza Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wazazi wote ambao hawajawapeleka watoto shule wanatafutwa popote walipo. Kwa kidato cha kwanza, hata mtoto asiye na viatu asikataliwe kuingia shuleni,” amesisitiza RC Mtanda.

Ameongeza kuwa walimu wanapaswa kushirikiana na wazazi wasio na uwezo wa kununua sare kwa kuingia makubaliano ya muda, ili kumpa nafasi mtoto kuendelea na masomo huku mzazi akitafuta namna ya kumfanisha na wenzake.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Bi. Ummy Wayayu, kwa kutenga shilingi milioni 60 kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara za shule hiyo na kufanikisha upatikanaji wa shilingi milioni 30 hadi sasa.

“Ninakupongeza kwa jitihada zako, lakini fedha iliyobaki ipatikane haraka iwezekanavyo ili mradi huu ukamilike kwa wakati,” amesema.

Mhe. Mtanda amehitimisha kwa kusema kuwa yuko tayari kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha fedha zinazotengwa zinatumika ipasavyo na kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AZINDUA SHULE YA SEKONDARI BUMYENGEJA KWIMBA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AZINDUA NYUMBA YA WATUMISHI KITUO CHA AFYA BUDUSHI, ATOA WITO KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.