• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA SENGEREMA DC KWENDA KUJIFUNZA TARIME DC UENDESHAJI MIRADI YA CSR

Posted on: November 25th, 2024

RC MTANDA AWATAKA SENGEREMA DC KWENDA KUJIFUNZA TARIME DC UENDESHAJI MIRADI YA CSR


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwenda kutembelea na kujifunza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara kuhusu upokeaji na uendeshaji wa fedha za Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) zinazotolewa na Migodi ya Dhahabu ili kuleta ufanisi na manufaa kwa wananchi wanaozunguka mgodi wa Sotta.

Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo mchana wa leo   Novemba 25,2024 wakati wa hafla ya kukabidhi Madawati 1131 na samani mbalimbali zenye thamani ya jumla ya Tshs. Milioni 93.8 vilivyotolewa na Mgodi wa Sotta mining Co. Ltd uliopo Wilayani Sengerema.

Akizungumza na wananchi baada ya makabidhiano hayo Mhe. Mtanda amewashukuru viongozi wa mgodi huo kwa kuwa sehemu ya jitihada za Serikali za kuwaondoa watoto kwenye adha ya kusongamana na kukaa chini kwa kuwapatia samani hizo.

Aidha, ameitaka Halmashauri hiyo kutoa elimu kwa vijiji ili wajiandae na kuunda kamati za Uwajibikaji wa Fedha za Kampuni kwa jamii (CSR) ili uzalishaji utapoanza waweze kukidhi kanuni zilizopitishwa na tume pamoja na wizara ya Madini.

"Na niwashauri tu muende mkajifunze kule Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Musoma na Butiama wao wameanza zamani wana uelewa wa kutosha kuhusu CSR na mimi nilikuwa huko kwa hiyo ninaelewa".

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Ndugu Binuru Shekidele amewashukuru na kusema mgodi umewapunguzia adha na kwamba kwa msaada huo watabaki na upungufu wa madawati elfu 12 tu kwa shule za msingi.

Kwa upande wake Afisa Mahusiano kutoka Kampuni ya Mgodi wa Sota Bi. Habiba Said Amesema madawati na samani hizo zimetolewa ikiwa na lengo la kuimarisha mahusiano kwa kuwa bado mgodi huo haujaanza kufanya kazi na wanatarajia kuanza kutoa CSR pindi mgodi huo utakapoanza uzalishaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.