• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI, AWATAKA WATUMISHI KUWAJIBIKA KUTUMIKIA WANANCHI

Posted on: March 12th, 2025

RC MTANDA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI, AWATAKA WATUMISHI KUWAJIBIKA KUTUMIKIA WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watumishi Mkoani humo kufanya kazi kwa kujituma katika kuwatumikia wananchi na kutimiza wajibu bila kusubiri kuagizwa ili kuleta tija kwa Taifa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo tarehe 12 Machi, 2025 wakati akihutubia baraza la wafanyakazi la watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Rock City Mall, Ilemela.

Amesema, mtu akifanya kazi kwa kujituma atapata mshahara kihalali na kwa Mwenyezi Mungu atapata thawabu kutokana na ibada aliyoifanya kupitia kuwajibika bila kuchoka.

"Watu wengi wanadai haki lakini hawatimizi wajibu, hiyo sio sawa kwanza ni dhuluma ni lazima kila mmoja abadilike na kuchapa kazi ndipo afurahie mshahara anaoupokea kutoka Serikalini." Amesisitiza Mhe. Mtanda.

Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni lazima wawe na mwenendo wa maadili wakati wote kuanzia mavazi hadi lugha wanazozitoa kwa wananchi ni lazima ziwe na staha pamoja na kuacha tabia za kukopa pesa ovyo. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Halikadalika, amebainisha kuwa katika bajeti ya mwaka 2024/25 Ofisi yake imetumia Milioni 171.6 kulipa madeni kwa watumishi 53 na kupandisha vyeo kwa watumishi 102 na amewahakikishia watumishi kuwa Serikali inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi.

Naye Mwenyekiti wa baraza hilo Bwana Balandya Elikana amesema baraza hilo lina manufaa makubwa ikiwemo kushirikisha wafanyakazi kutoa maoni na kupokea changamoto za watumishi na kuzifanyia kazi kupitia vikao mbalimbali vya kisheria hususan kwenye idara.

Awali, wajumbe wa baraza hilo walifanya uchaguzi ambapo bwana Gapchojiga Fabian ameshinda nafasi ya Katibu na Bi. Susan Ndunguru Katibu Msaidizi wa baraza hilo na mara moja viongozi hao wameanza miaka mitatu ya kutumikia nafasi zao kwa awamu ya pili mfululizo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.