Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA ARDHI KWA AJILI YA KUJENGA MAKAZI YA WAZEE

Posted on: June 10th, 2024

RC MTANDA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA ARDHI KWA AJILI YA KUJENGA MAKAZI YA WAZEE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amezitaka Halmashauri Mkoani humo kutenga maeneo maalum katika mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuhakikisha wanajenga makazi ya kulea wazee ili kuwahakikishia huduma bora.

Mhe. Mtanda ametoa rai hiyo wakati akizungumza na jumuiya ya wazee wa wilaya ya Sengerema katika mkutano wake alioufanya leo Juni 10, 2024 alipofanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na makundi mbalimbali wilayani humo.

"Sisi ni wazee watarajiwa, mipango yote tutakayoweka itatusaidia wenyewe siku za usoni hivyo ni lazima sasa tutenge maeneo ya kujenga makazi ya malezi na mwakani tuanze ujenzi ili wazee wakae sehemu moja na tupeleke huduma za kijamii." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amesema katika kuhakikisha wazee wanakua na malezi bora ni lazima familia iwajibike kuwatunza na watoto wawalee wazee maana wao tayari wamelelewa na kusomeshwa vizuri hadi kufika hapo walipo hivyo ni lazima wathamini upendo huo ambao pia unasisitizwa na maandiko ya dini.

Vilevile, ametoa wito kwa watumishi wa afya kuhakikisha wanatoa huduma za afya kwa wazee bila malipo kwa mujibu wa sera zetu na amezitaka familia kuhakikisha malezi ya mtoto yanaanza kwenye unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa zaidi ya miaka miwili na nusu ili kuwahakikisha afya njema.

Halikadhalika, amewataka wazee kuendelea kumuunga mkono Rais Samia kwa kumuombea awe na afya na siha njema kwani anaonesha kwa vitendo upendo wake kwa kundi hilo kwa kuwaboreshea huduma za afya ikiwepo uwepo wa madirisha ya wazee ya kuwahudumia kwa kipaumbele.

Mhe. Hamis Tabasam, Mbunge wa Sengerema amesema kuwa Jumuiya ya Wazee wilayani humo ina jumla ya wajumbe 640 na kwamba adha kubwa wanayoipata kwenye huduma za jamii ni gharama kubwa za matibabu hivyo wanaomba kupatiwa bima za afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.