• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

Posted on: January 26th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesisitiza umuhimu wa kuwepo kwa dhamira ya dhati miongoni mwa wajumbe wa Kamati ya Maadhimisho ya Sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 Kitaifa kutoka Mkoa wa Rukwa, akibainisha kuwa dhamira ndiyo nguzo kuu ya mafanikio ya tukio lolote la kitaifa.

RC Mtanda ametoa msisitizo huo wakati wa mazungumzo na wajumbe hao waliotembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kujifunza na kupata uzoefu wa maandalizi ya Sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa zitakazofanyika Mkoani Rukwa tarehe 14 Oktoba, 2026.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bw. Msalika Robert Makungu amesema wajumbe wa kamati wamegawanyika katika makundi mawili, kundi moja likitembelea Mkoa wa Manyara na lingine likiongozwa na yeye mwenyewe likitembelea Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kujifunza namna ya kuandaa na kusimamia sherehe za Kuzima Mwenge wa Uhuru.

RC Mtanda amesema kuwa ili sherehe za kitaifa zifanikiwe ni lazima kuzingatia mambo muhimu ikiwemo ushiriki wa wananchi kwa wingi, upangaji wa bajeti ya kutosha, urembo wa tukio kupitia matangazo na sare zinazovutia pamoja na uwepo wa mfumo mzuri wa uratibu na uendeshaji wa shughuli.

Ameongeza kuwa vikao vya kupanga na ushirikishwaji wa wadau ni muhimu ili kuhakikisha kila mmoja anakuwa na uelewa wa majukumu yake.

Akihitimisha, amewahimiza wajumbe wa Kamati ya Maadhimisho ya Mwenge wa Uhuru 2026 Mkoa wa Rukwa kujitoa kwa moyo wote, akisisitiza kuwa kujituma hakufundishwi bali hutokana na dhamira binafsi na ushirikiano wa pamoja.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.