• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC .Mwanza aongoza Mafunzo Watumishi wa Halmashauri ya Misungwi namna ya utoaji fedha za Mikopo

Posted on: May 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Mhandisi Robert Gabriel ameongoza mafunzo kwa Watumishi wa Halmashauri ya Misungwi yanayohusu namna ya utoaji na matumizi sahihi ya fedha za  Mikopo ya asilimia kumi zinazotolewa na Halmashauri kwa Makundi maalum.


Zoezi hilo la Mafunzo linafanyika ikiwa ni maelekezo yake aliyotoa Aprili 25 mwaka huu baada ya kutangaza kusimamisha utoaji wa Mikopo hiyo  kutokana na kubainika Halmashauri kufanya ubadhirifu wa fedha wakati wa utoaji wa Mikopo hiyo.


Mafunzo hayo yanayotolewa na timu ya Wataalamu wa masuala ya Miradi na Tathmini,TAKUKURU na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,yamelenga kuwaelimisha sheria na kanuni za namna ya utoaji wa Mikopo hiyo.


Mkuu wa Mkoa Mhandisi Gabriel amesema fedha hizo za Mikopo ipo ndani ya Ilani ya Uchaguzi kuyalenga Makundi maalum kujikwamua na tatizo la ajira.


"Wilaya hii ya Misungwi ni miongoni mwa zilizopata tatizo la ubadhirifu wa utoaji wa Mikopo, fedha iliyorejeshwa hadi sasa ni Milioni 57 bado Bilioni 4.3" amesema Mkuu huyo wa Mkoa.



Kwa upande wake Mkuu wa Dawati la kuzuia rushwa Mkoa wa Mwanza,Stella Bukulu amesema katika uchunguzi wao wamebaini mapungufu mengi kwa Idara zilizohusika na utoaji wa Mikopo hiyo ama kwa kutokujua au uzembe.


Prudence Sempa ambaye ni Mtaalamu wa masuala ya Miradi na Tathmini kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, amefafanua Sheria kadhaa kwa Vikundi vinavyotaka fedha za Mikopo.


Washiriki wa mafunzo hayo ni Kamati za fedha na mipango,Wakuu wa Idara kutoka Halmashauri ya Misungwi,pamoja na Watendaji kata wote kutoka ndani ya Halmashauri hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Mhandisi Robert Gabriel anasimamia mafunzo hayo kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza baada ya kubainika ubadhirifu wa fedha za mikopo za asilimia kumi ambazo zimewalenga Makundi ya Vijana,Wanawake na watu wenye ulemavu..


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.