• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MWANZA ASIKILIZA KERO ZA WAMACHINGA,VIONGOZI WA MASOKO NA MINADA MKOANI MWANZA

Posted on: September 14th, 2023

RC MWANZA ASIKILIZA KERO ZA WAMACHINGA,VIONGOZI WA MASOKO NA MINADA MKOANI MWANZA


*Awataka Machinga kufanya biashara kwenye maeneo waliyopangiwa*


*Aaagiza kuwepo dawati la kusikiliza kero za wafanyabiadhara kila Halmashauri*


*Aitaka LATRA kuweka utaratibu wa mizunguko ya mabasi kwenye masoko ili kuwe na muingiliano wa watu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amekutana leo viongozi wa makundi ya wafanyabiashara kwa lengo la kusikiliza kero zao na kutoa maagizo kumi likiwemo la kuwasisitiza kufanya biashara zao kwenye maeneo waliyopangiwa huku mikakati ya kuboresha maeneo yao ikiendelea kufanyiwa kazi.

Akizungumza na makundi ya wawakilishi hao kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ametoa maagizo likiwemo la kuzitaka Halmashauri zote Mkoani humo kuwa na dawati la kusikiliza kero za wafanyabiashara hao ambalo litasaidia kuzitatua changamoto zinazowakabili za mara kwa mara.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ana uzoefu na changamoto za wafanyabiashara kutokana na kufanya kazi kwenye majiji kadhaa nchini amewaagiza kila Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na Maafisa biashara kuweka mpango mkakati wa kuboresha masoko katika maeneo yao.

"Nawaagiza pia LATRA kuhakikisha wanaweka mpango wa mizunguko ya mabasi kupita kwenye masoko yote ili kuwepo na muingiliano wa watu na biashara iweze kufanyika kwa tija, haiwezekani kuwaweka wafanya biashara kwenye maeneo ambayo hakuna muingiliano wa watu, wataishia kuyakimbia masoko wakihofia mitaji yao kukatika, LATRA mzingatie hilo,"CPA Makalla.

Kuhusu miundombinu Mkuu huyo wa Mkoa ametoa agizo kwa TARURA kuboresha barabara zote maeneo ya masoko ili kuhakikisha zinapitika kwa urahisi ili shughuli za kupeleka mizigo na wanunuzi zifanyike kwa wepesi.

Aidha, Makalla amewakumbusha Wakuu wa Wilaya kuwa na vikao vya mara kwa mara na wafanyabiashara hao hali ambayo itasaidia kuzitambua kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa haraka.


Kuhusu Soko kuu lililopo katikati ya Jiji linalotarajiwa kukabidhiwa kwa Serikali Disemba mwa mwaka huu, Mhe.Makalla amewahakikishia kipaumbele kitatolewa kwa wafanyabiashara wa awali ambao walikuwepo kabla ya kupisha mradi huo kufanyika.

Vilevile, Mkuu huyo wa Mkoa ametoa rai kwa wafanyabiashara hao kuwa na umoja na kudumisha amani katika shughuli zao na amewaahidi kuwa na vikao nao vya mara kwa mara ili kusikiliza changamoto zao na kuzifanyia kazi.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa Wilaya yangu Ina jumla ya wafanyabiadhara 12,850 na masoko 15 licha ya changamoto za hapa na pale lakini biashara zao tunahakikisha zinafanyika katika mazingira mazuri," Amesema Mhe.Amina Makilagi,Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana.

."Wilaya ya Ilemela tuna jumla ya wafanyabiashara 3500 na masoko 8 yaliyo rasmi na yasiyo rasmi lakini tumekuwa makini kuhakikisha wafanyabiashara hao wanatii bila shuruti miongozo iliyopo,"Mhe.Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.