• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza azitaka Halmashauri kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha

Posted on: June 28th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, ametoa siku 90  kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuwatafuta watumishi 53 ambao wamelipwa mishahara Jumla ya Tshs Milioni 486 kwa mwaka wa fedha 2015/16 wakati wakiwa wameshastaafu.

Mhandisi Gabriel ametoa agizo hilo leo Juni 28, 2022 baada ya kuibuka hoja katika kikao Maalum cha Madiwani cha kujadili Utekelezaji wa Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambapo Afisa Utumishi wa halmashauri hiyo Mang'oha Maginga alisema awali walikuwa wanadai Tshs milioni 657 kwa watumishi waliolipwa fedha wakiwa wamestaafu na wengine wakiwa wamefariki.

Ndugu Maginga aliendelea kufafanua kwamba baada ya kufuatilia kwa kina watumishi 21 walirejesha Tshs Milioni 111.1 hivyo deni lililobaki ni Tshs Milioni 486 ambazo wanadaiwa watumishi 53 ambao wako hai huku watumishi 21 waliofariki dunia wakiacha deni la shilingi milioni 63.

"Hawa watu wapo katika mfumo wa malipo ya mifuko ya hifadhi ya jamii na wana namba za hundi za malipo hivyo kutokuwafualia kwa kipindi chote hicho ni uzembe wa hali ya juu yaani haiingii akilini mnakuja kuwabaini leo kwenye kikao, sasa nahitaji ndani ya siku 90 fedha hizo za Umma zirudi." Mhandisi Gabriel.

Baada ya kuibuka hoja ya kudaiwa zaidi ya Tshs Bilioni 1 zilizokopwa kutoka kwenye Akaunti ya Amana, Mhe Mkuu wa Mkoa amewaagiza Halmashauri hiyo kuacha tabia ya kukopa fedha na badala yake amewataka kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha ili kujiendesha kutokana na Mapato ya Ndani.

Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Mwanza, Waziri Shabani amefafanua kuwa kwa hesabu za mwaka wa Fedha 2020/21 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe imepata Hati Inayoridhisha.

Mkutano Maalumu wa  kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG katika halmashauri ya wilaya Ukerewe umehitimisha ziara ya Mhandisi Gabriel ya kujadili hoja katika Halmashauri zote za mkoa wa Mwanza zilizoanza juni 20 mwaka huu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.