• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI IMETENGA BILIONI 4 KUJENGA HOSPITALI YA MKOA YA RUFAA UKEREWE: WAZIRI UMMY

Posted on: March 13th, 2024

SERIKALI IMETENGA BILIONI 4 KUJENGA HOSPITALI YA MKOA YA RUFAA UKEREWE: WAZIRI UMMY


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali imenuia kuondoa adha ya matibabu kwa wakazi wa Ukerewe na visiwa vya jirani kwa kutenga shs bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya mkoa ya Rufaa wilayani humo.

Akitoa taarifa fupi leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya afya na masuala ya ukimwi Waziri Ummy amebainisha kuwa Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kwa vitendo kuwaletea wananchi maendeleo ikiwemo kuiboresha sekta ya afya.

"Ndugu mwenyekiti wa kamati nimesimama hapa kutoa taarifa fupi ya Serikali, usumbufu wa matibabu na hata vifo kutokakana na jiographia ya Ukerewe sasa basi, naomba fedha zitakapofika Ofisi ya mkuu wa Mkoa mfanye usimamizi mzuri ili mradi huu wa ujenzi ukamilike kwa wakati na uwe na tija kwa wananchi", amesisitiza Mhe. Ummy

Kuhusu suala la upungufu wa watumishi zaidi ya elfu kumi kwenye sekta ya afya, Waziri Ummy ameziagiza Halmashauri zote mkoani humo kutumia mapato yao ya ndani kuwaajiri watumishi kwa mikataba wakati utaratibu wa ajira rasmi kutoka Serikali kuu  ukiendelea kufanyika.

Waziri Ummy pia amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa usimamiaji mzuri wa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu na kuhimiza utoaji wa elimu uzidi kuzingatiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema Mkoa huo umepokea jumla ya shs bilioni 48 ambazo ni gharama ya miradi ya afya na akaahidi kutaendelea kuisimamia ili iwe na tija kwa wananchi.

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya afya na masuala ya ukimwi ambaye pia ni Mbunge wa Maswa Mashariki Mhe. Stanslaus Nyongo amesema jukumu la kamati yake ni kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali zimetumika kwa malengo yaliyokusudiwa na pia kuishauri Serikali mpango sahihi wa kuwaletea maendeleo wananchi.


"Hospitali ya Sekou Toure tangu ilipoanza kuwa ya rufaa imezidi kupiga hatua kwa kutoa huduma bora na za kibingwa hasa baada ya Serikali kuzidi kuiboresha.

"Mhe Mwenyekiti wa kamati hospitali ya Sekou Toure sasa hivi tunatoa huduma za kusafisha damu pia Serikali imewasomesha Madaktari 17 tabibu za kibingwa lengo likiwa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi", Dkt. Bahati Msaki, Mganga Mfawidhi Sekou Toure.

Kamati hiyo ya Bunge itahitimisha ziara yake alhamisi ya hii kwa kutembelea Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya Bugando.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.