• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI ITAENDELEA KUTHAMINI MCHANGO WA WANASAYANSI NCHINI - DKT. BITEKO

Posted on: November 13th, 2024

SERIKALI ITAENDELEA KUTHAMINI MCHANGO WA WANASAYANSI NCHINI - DKT. BITEKO


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema  Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na kuwajengea mazingira mazuri wanasayansi nchini ili kuenzi mchango wao katika kuimarisha sekta ya afya.

Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Novemba 13, 2024 wakati akifungua Kongamano la Kimataifa la Sayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Sayansi (CUHAS) katika hoteli ya Malaika Ilemela Mwanza.

Amesema wanasayansi wana mchango mkubwa katika kukabili majanga ya kiafya mathalani maradhi ya mlipuko kupitia tafiti zao wanazofanya ambazo zinatoa majibu ya chanzo na namna ya kukabiliana na maradhi fulani kupitia machapisho wanayotoa.

Aidha, amewapongeza Chuo Kikuu cha Sayansi Bugando kwa kutoa zaidi ya machapisho 150 ya kisayansi yanayotoa mchango mkubwa kwenye upangaji wa sera nchini na kwa kipekee Prof. Steven Mshana ambaye ameibuka kuwa mwanasayansi bora wa mwaka 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema wananchi wa Mkoa huo wanaishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Tanzania kwa kuupatia Mkoa huo fedha zaidi ya Tshs. Trilioni 6 kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Vilevile, amebainisha kuwa wananchi wa Mkoa huo wanajivunia uwepo wa Ziwa Victoria ambalo wanalitumia kuwainua kiuchumi katika shughuli za uvuvi na kwamba wananchi wake wana afya njema wanaendelea kuchangia pato la Taifa kwa zaidi ya asilimia 7.2.

Kongamano hilo la 14 lililoandaliwa na hospitali ya kanda ya rufaa Bugando na chuo kikuu cha sayansi kimewakutanisha zaidi ya wataalamu 450 kutoka ndani na nje ya nchi wanaokutana kujadili mustakabali wa magonjwa na namna ya kuyakabili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.