• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI YAIMARISHA SEKTA YA ARDHI KUPITIA TEHAMA

Posted on: January 27th, 2026

Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuleta mageuzi katika Sekta ya Ardhi nchini kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ikiwa ni jitihada za kuboresha utoaji wa huduma na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Katika hatua hiyo, Serikali imetumia zaidi ya shilingi bilioni 5 kununua jumla ya vifaa vya TEHAMA 1,429 ambavyo vitasambazwa katika Halmashauri 184 kote nchini.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika leo Januari 27, 2026 kwa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mwanza, Bw. Wilson Luge, amesema mkoa huo umepokea jumla ya vifaa 61.

Amesema kwa wastani kila Halmashauri imepatiwa kompyuta mbili, printa moja pamoja na UPS mbili, huku Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikipewa vifaa vya ziada ikiwemo kompyuta mbili zenye skrini, pamoja na simu za mezani kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano.

“Ni uwezeshaji mkubwa uliofanyika. Tunaamini kuongezeka kwa vifaa hivi kutapunguza changamoto ya uhaba wa vifaa uliokuwepo awali na kuboresha kwa kiasi kikubwa utendaji kazi,” amesema Bw. Luge.

Ameongeza kuwa Sekta ya Ardhi kwa sasa inatumia mfumo wa kielektroniki wa e-Ardhi, unaolenga kurahisisha na kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi, na kwamba vifaa hivyo vitasaidia kuongeza kasi na ufanisi wa mfumo huo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amesema Serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuboresha miundombinu ya utoaji huduma katika sekta mbalimbali, ikiwemo Sekta ya Ardhi, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.

“Vifaa hivi ni vingi na vimetumia gharama kubwa. Hata hivyo, havitakuwa na maana endapo huduma zitabaki kama zilivyokuwa awali. Matarajio yetu ni kuona maboresho ya dhahiri katika utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema Bw. Balandya.

Katika hatua nyingine, Katibu Tawala ametoa onyo kwa watendaji wa sekta ya ardhi akisema hatarajii kuona vibali vya ujenzi vinatolewa katika maeneo yasiyoruhusiwa, wala kuwepo kwa umiliki wa ardhi kwa zaidi ya mtu mmoja, akibainisha kuwa mifumo ya kidijitali itaondoa changamoto hizo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

    January 29, 2026
  • HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • TRA MWANZA YATOA MAFUNZO YA MFUMO JUMUISHI WA KODI ZA NDANI KWA WAFANYABIASHARA

    January 28, 2026
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI WA WIZARA YA ULINZI NA JKT MWANZA

    January 28, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.