• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali yatoa maelekezo kwa TPA kuboresha Bandari zake Ziwa Viktoria ili MV Mwanza itoe huduma bora

Posted on: February 12th, 2023


Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Atupele Mwakibete, ameitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) kuhakikisha inaendelea kuboresha bandari katika Ziwa Viktoria ili meli mpya ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu iweze kutia nanga bila shida wakati itakapoanza safari zake.

Mwakibete ametoa maelekezo hayo leo Februari 12, 2023 jijini Mwanza baada ya kushuhudia meli hiyo  kubwa  ambayo itakuwa na mwendokasi zaidi kuliko meli zote zilizopo nchini ikiingizwa majini kwa mara ya kwanza katika bandari ya Mwanza Kusini  iliyopo Wilaya ya Nyamagana itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200 na tani 400 za mizigo kwa wakati mmoja inayojengwa na mkandarasi  kampuni ya GAS Entec ya Korea Kusini kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 109.

.Amesema Serikali imekuwa ikiwekeza kwenye miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ya  usafiri nchini lengo ni kuboresha huduma za usafirishaji wa mizigo na abiria kwa wananchi wake hivyo itakapoanza kufanya safari zake kusiwepo na changamoto ya bandari kwenye maeneo itakayopita.

“Pia naielekeza Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Huduma za Meli(MSCL) kusimamia vyema menejimenti ya MSCL ili miradi yote inayotekelezwa na itakayotekelezwa na Serikali ileta thamani halisi ya fedha iliyowekezwa ikiwa ni pamoja na kuendelea kusimamia mradi huu wa Ujenzi wa Meli ya Mv Mwanza Hapa Kazi Tu  ukamilike ndani ya muda uliopangwa ili meli hii ianze kuwahudumia wananchi mapema iwezekanavyo,” amesisitiza Mhe. Mwakibete.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa MSCL, Mhandisi Eric Hamissi  ujenzi wa Meli hiyo ambayo  itafanya safari zake katika nchi zote ambazo ziko ukanda wa ziwa viktoria umekamilika kwa asilimia 82 na asilimia 12 zilizobaki zinatarajiwa kukamilika ndani ya miezi minne hadi mitano kuanzia sasa  na kwamba hakuna changamoto ya fedha kwani hadi sasa Mkandarasi amekwishalipwa asilimia 88 ya gharama zake sawa na Sh bilioni 93.8 fedha iliyobaki tayari ipo kwenye akaunti wanasubiri  amalize kazi ili waweze kummalizia malipo yake.


Amesema  meli hiyo ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu  ina urefu wa mita 92.6, kimo ghorofa nne, upana mita 17  pia itakuwa na mwendo kasi tofauti na zingine zote ambazo zinafanya safari zake katika maziwa makuu hivyo itarahisisha  shughuli  za usafiri na usafirishaji kwa abiria na mizigo.

“Meli ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu ikikamilika itakuwa ni kivutio kizuri sana  tunataka watu wasafiri na kufanya utalii wakiwa safarini kwani ni ya tofauti kabisa itakuwa na uzito wa Tani 3500 leo tumeingiza majini tani 3000 hii ndiyo meli kubwa kuliko zote zinazoelea katika ukanda wa maziwa makuu.

“Hii Meli itakapokamilika itakuwa na madaraja sita ikiwemo daraja la hadhi ya juu kabisa(VVIP)  daraja la watu mashuhuri(VIP),daraja la kwanza(first class) litabeba watu  60, daraja la pili (second class )abiria 200, daraja la biashara(business) abiria 100, daraja la uchumi lenyewe litakuwa na uwezo wa kubeba abiria 834.

“Kutakuwa na lifti ambayo inauwezo wa kubeba watu 20 kwa wakati mmoja kwa ajili ya abiria ambao wanachangamoto ya kupanda ngazi na wagonjwa, migahawa ya kisasa, sehemu ya kucheza muziki, dispensary, ukumbi wenye uwezo wa kubeba watu 400 ambao wanaweza kufanyia sherehe humo kwa hivyo itakuwa ni kivutio kizuri sana ,,”ameeleza  Mhandisi Hamissi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika hafla hiyo ya kusushwa majini kwa Meli ya Mv Mwanza Hapa Kazi Tu, Wakuu wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa  walisema kutekelezwa kwa mradi huo ambao umekuwa ni ndoto ya muda mrefu ya wananchi wao kunatarajiwa kuchagiza maendeleo ya wananchi na uchumi wa taifa kwa ujumla kwani usafiri wa meli ni wa gharama nafuu zaidi pia unawezesha kusafirisha shehena kubwa kwa wakati mmoja.

“Wakazi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa tunakila sababu ya kumshukuru Rais wetu  Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan  kwa uamuzi wake wa kuendelea kuwekeza fedha nyingi sana katika mradi wa Meli ya Mv Mwanza Hapa Kazi Tu pamoja na miradi mingine ya maendeleo ya kimkakati iliyopo mikoa ya kanda ya ziwa,”amesema Mhe. Adam Malima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.