• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Shirika la AGPAHI latoa msaada wa kujikinga dhidi ya CORONA

Posted on: June 18th, 2020

Licha ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na kirusi aina ya Corona (COVID-19) kupungua wananchi  Mkoani Mwanza wameombwa kuendelea kuchukua tahadahari huku shirika la AGPAHI likitoa msaada wa vifaa vya kupimia joto kwa ajili ya uchunguzi wa awali wa ugonjwa huo.

Ambapo AGPAHI imekabidhi jumla ya mashine 100 zenye thamani ya milioni 25 kupitia ufadhili wa taasisi  ya CDC kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ambavyo vimepokelewa na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Emmanuel Tutuba.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Emmanuel Tutuba, amemshukuru Mungu kuwa kwa sasa Mkoa huo, maambukizi ya Corona yamepungua lakini wanaendelea kusisitiza  watu wote waendelee kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.

Tutuba anasema, endapo kutakuwa  na mgonjwa au mtu mwenyewe anayejihisi  kuwa na dalili mbalimbali za awali za  ugonjwa huo asisite kwenda kwenye kituo cha kutolea huduma za afya ili wataalamu waendelee na vipimo na hatimaye kumpatia matibabu.

Pia anasema,wameendelea kuwasisitiza watoa huduma kuendelea kutoa huduma bila unyanyapaa huku wananchi wakitakiwa kuchukua tahadhari kwa kunawa mikono na maji tiririka, sabuni na kutumia vitakasa mikono na kuendelea kuzingatia maelekezo mbalimbali ikiwemo kukaa umbali wa mita moja kutoka mtu mmoja hadi mwingine.

Tutuba alilishukuru shirika hilo pamoja na wadau wengine wanaounga mkono kwa kuwezesha vifaa mbalimbali wanavyovitoa ambapo walikuwa na kiu kubwa sana kwani katika vikao mbalimbali walikuwa wakiongelea namna ya kufanya uchunguzi wa awali ili kubaini nani mwenye dalili za awali kupitia joto linalozidi kiwango ili kusudi aendelee kupata huduma nyingine za kimatibabu endapo atakuwa ameshukiwa kuwa na ugonjwa huo.

"Nitumie fursa hii kuwashukuru sana kwa msaada huu ambao mmeutoa wakati muafaka kwani bado vinahitajika,kama sekretarieti ya Mkoa tuna ahidi kwamba mashine hizo zitagawiwa kwenye maeneo yote ambayo Mkuu wa Mkoa ameisha yaainisha na zitatumika kwa uangalifu na kwa mahitaji yaliyokusudiwa,"anasema Tutuba.

Kwa upande wake Meneja Mipango wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa Dkt.Nkingwa Mabelele anasema wamekuja kukabidhi vifaa hivyo vyenye thamani ya milioni 25 ambavyo vitatumika kupima joto la mtu ili kubaini mwenye joto la juu ambaye inawezekana akawa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TAMISEMI ilivyotumia Wiki ya Kitaifa ya Usalama Barabarani Mkoani Mwanza kwa kutoa huduma mbalimbali kwa jamii

    March 22, 2023
  • RC Malima ataka adhabu kali na marekebisho ya Sheria za barabarani dhidi ya wanaosababisha ajali kwa uzembe

    March 17, 2023
  • Tupo katika mchakato wa Katiba mpya-Mhe.Dkt.Ndumbaro

    March 17, 2023
  • Miaka miwili ya Rais Samia madarakani,Mwanza yajivunia kasi ya miradi ya maendeleo

    March 15, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.