• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Taasisi za Bima zaaswa kujikita maeneo ya vijijini

Posted on: September 26th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella  ameziagiza taasisizinazojihusisha na masuala ya  bima nchini kujikita zaidi maeneo yavijijini kutoa elimu badala ya kupigana vikumbo  mjini  wakigombaniawateja ambako  wananchi wana uelewa na kipato cha kujitibu mudawowote.

Agizo hilo alilitoa jana  wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya bimayanayofanyika kitaifa mkoani Mwanza katika viwanja vya  jengo labiashara la kimataifa la Rocky City Mall ambapo alisema anashangazwa kuonataasisi za bina zikiendelea  kupambana katikati ya mjini wakativijijini kuna uhitaji mkubwa.

"Kama tunavyojua sekta ya bima ni sekta nyeti, muhimu na ina mchangokwenye uchumi wa taifa,  ninatambua kuwa taasisihizi  zinafanya kazi kubwa  kwa ni  bima yenyeweina faida nyingi sana kwa sababu ili biashara na shughuli zote za uzalishajimali ziwe na uhakika wa usalama kimsingi zinatakiwa kukatiwa bima.

"Hivyo niwaombe  endeleeni  kutoa elimu kwa watu wamakundi yote kwani kuna baadhi yao  bado wanamini na wanaichukuliabima kama gharama na  kusahau  kuwa unapokuwa na bimaunakuwa kwenye mikono salama.

"Labda tu niwakumbushe wananchi wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla bimani gharama ila unapokuwa nayo  unakuwa na amani muda wote, hatalikitokea janga au ajali yeyote kwenye biashara, vyombo vya usafiri na hatakwenye nyumba yako hautahangaika sana.

"Lakini pia kuna changamoto moja taasisi hizi za bima nanyimmerundikana mjini, ofisi zenu zipo Dar es salaam huku mikoani haumpo, ilimuwafikie wananchi wengi zaidi basi mjitahidi kuwekeza nguvunyingi  maeneo ya vijijini, mkifanya hivyo elimu ya bima itaenea nchinzima na itakuwa na msaada kwa watu wote," alisema Mongella.

Mongela alisema  ni ukweliusiopingika  juhudi  za elimu kwa bima zinaonyesha matundayake katikati ya mijini ispokuwa vijijini  ambapoalisisitiza  wakuu wa taasisi  hizo kubadili mwelekeo nakuifuata jamii inapoishi.

Alisema kama mkuu wa mkoa amekuwa akitembelea vijiji  na kuonahalisi ya jamii kutokuwa na elimu ya bima na wanapoelezwa wanaonyesha kuwa nauhitaji, hivyo  ni wakati muafaka taasisi hizo kutambua asilimia 80ya watanzania wapo vijijini  na kusisitiza kuwa lengo la Serikali nikufikia asilimia 50 kila mtanzania kuwa na bima ifikapo 2028.

Kwa Upande wake Rais wa Taasisi za Bima Tanzania (TIRA), James Bosco alisemakuwa ameguswa na maneno ya Mongela na kuahidi kwamba kuanzia sasa ataelekezanguvu kubwa  ikiwa lengo ni kuhakikisha wanaifikisha elimu ya bimakwa kila mtanzania.

"Kuwa na  bima ni kitu muhimu kwenye maendeleo ya uchumi wataifa lakini tumegundua kuwa katika pato la taifa bima bado haina mchangomkubwa, sasa ni wajibu wetu tulio ndani ya bima kutoa elimu ili watu wengizaidi waweze kuelewa shughuli zetu.

"Pamoja na kuyatumia maonyesho haya pia tunaahidi tutayafikia maeneoyote nchini ikiwamo vijijini ambavyo  kwa kiasifulani  hatujawahi kuonekana,  hapa Mwanza tunatambua kuwakuna wavuvi na wakulima wengi hivyo watu kama hao wasijihisi kama bima haiwahusubali wanatakiwa wakate bima ili yanapotokea majanga yasiyotarajiwa na kupotezamali zao wasije wakaanza upya," alisema Bosco.

Kwa upande wake Kamishina wa Bima Tanzania, Musa Juma alieleza kuwa hadisasa asilimia 34 tu ya Watanzania ndio wenye uelewa na bima hivyo wao kamataasisi za bima wanaendelea kutumia njia mbadala hasa mitandao ya kijamii naujumbe wa simu ili kuongeza uelewa zaidi kuhusu bima nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.