• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TAASISI ZOTE MWANZA ZATAKIWA KUJISAJILI PDPC

Posted on: March 28th, 2025

TAASISI ZOTE MWANZA ZATAKIWA KUJISAJILI PDPC


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amezitaka Taasisi zote za Umma na binafsi Mkoani humo kuhakikisha wanajisajili katika Mfumo wa Usajili na Uzingatiaji wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC )kabla ya Tarehe 30 Aprili, 2025 ambayo ni ukomo wa kujisajili kwa hiari baada ya muda wa nyongeza uliotolewa na Tume.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mhe. Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wakati wa kufunga Warsha maalumu kwa Kamati ua Usalama Mkoa pamoja na Wadau wa Taasisi za Umma na Binafai leo machi 28, 2025.

Mhe. Mtanda amesema baada ya tarehe hiyo ya ukomo taasisi zote zitakazoshindwa kujisajili zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni na sheria za kiutawala.

“Na nitumie nafasi hii kumuagiza Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha barua hizo ulizoletewa kutoka Tume kuhakikisha zinazifikia Taasisi zote kwa utekelezaji”.

Aidha, ameziagiza pia Taasisi zote za Umma na Binafsi kuteua Maafisa wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi (DPOs) ambao watahusika moja kwa moja na usimamizi wa ulinzi wa taarifa binafsi ndani ya Taasisi zao kwa mujibu wa matakwa ya Sheria ya ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuwa usalama wa taarifa binafsi ni msingi wa maendeleo ya kidigitali na uaminifu katika utoaji huduma nchini, hivyo ametoa rai kwa washiriki hao kutumia fursa hiyo kujifunza kushirikiana na kubadilishana uzoefu ili kuimarisha mifumo ya ulinzi wa taarifa binafsi Mkoani Mwanza.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa PDPC Dkt. Emmanuel Mkilia amesema Mkoa wa Mwanza ni Mkoa unaokua kwa kasi na kuna umuhimu mkubwa wa utekekezaji wa sheria hiyo ambapo kwa sasa ni Taasisi 20 pekee ndio wamejisajili hali inayotakiwa kubadilika ili Mkoa pia utajwe kuwa mfano katika ulinzi wa taarifa binafsi

Aidha Tume hiyo imemuomba Mkuu wa Mkoa kuhamasisha Taasisi hizo kufanya warsha kwa watumishi wao ili kuongeza uelewa wa ulinzi wa taarifa binafsi na wajibu wa Taasisi katika kulinda utu na faragha za watu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.