Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA Yafanya Ziara ya kushtukiza usajiri wa laini mfumo wa Biometric

Posted on: May 2nd, 2019


MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imefanya ziara ya kushtukiza katika kampuni tano za mawasiliano kwa lengo la kuona  namna ya zoezi la usajili wa laini kwa kutumia mfumo wa alama za vidole(Biometric) linavyofanyika huku  wananchi wakifurahia jinsi wanavyohudumiwa licha ya kuwapo na msongamano mkubwa.

Ziara hiyo iliyoongozwa na Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Francis Mihayo na watumishi wenzake watano pamoja na waandishi wa habari huku wakitembea kwa miguu, walianzia ukaguzi kampuni ya Halotel  na kukagua mashine za usajili zinavyofanya kazi na kuwahoji wananchi wanaosajiliwa.

Pia  walikwenda kampuni ya  Airtel, Vodacom, Tigo, Smile na TTCL  ambapo licha ya kuwapo na kasoro ndogo ndogo za kimtandao,  zoezi hilo lilionekana kuwafurahisha wananchi baada ya Mhandisi Mihayo kutoa maelekezo kwamba wananachi wote wenye vitambulisho  tofauti na vile kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) nao wasajiliwe na kuwapa elimu kwamba usajili huo  ni wa muda ambapo unakoma Desemba mwaka huu.

Changamoto  ndogo  zilioonekana kutoka kwenye baadhi ya  kampuni zilizotembelewa ni mashine zinazochukua alama za vidole kutokuwa na mawasiliano ya kutosha kati yao na NIDA kitendo ambacho kinasababisha wananchi kukaa muda mrefu kwenye foleni.

Vile vile baadhi ya vyumba wanapofanyia usajili huo kuzidiwa na watu ambapo wengine hulazimika kupanga foleni nje  ambapo Mhandisi Mihayo ameelekeza kila kampuni kuongeza mashine ili kurahisisha zoezi hilo na pale wanapohitaji msaada wowote wasisite kufika TCRA.

Hata hivyo wananchi wengi waliomba kampuni kuweka utaratibu wa kuwahudumia wazee na akina mama wenye watoto na wajawazito ili kuepuka kukaa muda mrefu kwenye foleni, pia waliomba usajili huo ufanyike maeneo mablimbali kuepusha gharama za kusafiri kwenda mjini.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara hiyo, Mhandisi Mihayo, alisema lengo ni kusimamia utekelezaji wa usajili wa laini kwa mfumo wa biometric na kuona linavyofanyika na changamoto zake ingawa tathimini ya haraka tunaweza kusema zoezi linakwenda vizuri sana.

“Kikubwa tulichokuiona ni mwitiko kuwa mkubwa na kusababisha foleni, sasa hapa nilipo nafikiria siku ya kuwaita viongozi wa kampuni hizo kwa kanda ya ziwa ili waje hapa tupange namna ya kuongeza vituo vya usajili, tumeshuhudia pale Airtel na voda watu walivyokuwa wengi.

“Rai yangu kubwa kwa watanzania tusisubiri zoezi hili mpaka ifike Desemba ndio tujitokeze kwenda vituoni, tutakuwa tumechelewa naomba wananchi pale anapopata nafasi akasajili laini yake, wenye vitambulisho vya NIDA wao watapata usajili wa kudumu na si lazima uende na kitambulisho hata namba zenyewe zinatosha.

“Wale wenye vitambulisho vingine kama leseni ya udereva, kadi ya mpiga kura na vingine vilivyoruhusiwa hao watasajiliwa kwa usajili wa muda hadi Desemba, baada ya hapo namba  usajili huo utafutwa, leo nimefanya ziara hii mjini lakini najipanga kwenda vijijini katika mikoa yote ya Kanda ya Ziwa,”alisema.

Naye Meneja Huduma kwa Wateja Kanda ya Ziwa kutoka Kampuni ya Tigo, Beatrice Kinabo alisema mpaka sasa wana maduka mawili jiji la Mwanza ya  usajili na huku Ukerewe likiwapo moja ambapo kwa siku wanasajili zaidi ya wateja 100.

Kinabo alisema kwa Mkoa wa Mwanza wana mashine  zaidi ya saba  zinazotumika kusajili wateja wao ambapo nguvu sasa ipo katikati ya Jiji la Mwanza na baadaye watakwenda wilayani.

Kwa upande wa Mtendaji Kiongozi wa Kanda ya Ziwa kutoka Vodacom, Dominishan Mkama alisema kwa siku ya juzi walisajili wateja 250 lakini jana mashine ilionekana kuwa na kasoro wakati wakiendelea na zoezi hilo ambapo alifafanua kwamba tayari amewasiliana na NIDA na kuahidiwa kulitatua haraka.

Naye Meneja wa TTCL Mkoa wa Mwanza, Jalili Bakari alisema zoezi  hilo linakwenda vizuri ingawa changamoto ndogo ndogo za kimtandao zinasumbuaa ambapo kwa  siku wanasajili watu 100 na kuendelea, hivyo aliomba NIDA kushirikiana pale inapotokea tatizo.







Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.