• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA yatoa msaada wa Kompyuta Buchosa

Posted on: June 22nd, 2018


Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imetoa msaada wa kompyuta 12 katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza ili kuhakikisha jamii za pembezoni zinanufaika na maendeleo ya sekta ya teknolojia  ya Habari na mawasiliano(TEHAMA).

Akiongea wakati wa uzinduzi wa kituo hicho cha TEHAMA (TELESENTA) Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Mhandisi James M. Kilaba amesema kuanzishwa kwa kituo hiki ni faraja kwa TCRA kwani wamekuwa wakianzisha vituo kama hiki maeneo mbalimbali nchini na vimeleta tija kwa wananchi kwani vimechangia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

“TEHAMA imeleta mafanikio makubwa kwani wateja na watoa huduma wameongezeka katika eneo la simu za viganjani,huduma za intaneti,vituo vya televisheni na redio na ongezeko la huduma za kifedha kupitia simu za mikononi,”alisema Mhandisi Kilaba.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella katika uzinduzi wa kituo hicho amesema kuwa dunia sasa inaelekea kwenye uchumi wa kidijitali ambapo TEHAMA ni nyenzo muhimu ya kufikia maendeleo ya kiuchumi hivyo ni vema Nchi kuwekeza katika TEHAMA hususani kuijengea uwezo jamii ili iweze kukabiliana na mabadiliko haya ya utandawazi.

Hata hivyo Mhe.Mongella ameipongeza Serikali kwa juhudi inazofanya na kuwashukuru TCRA kwa kufanikisha kuanzishwa kwa kituo hicho,pia amewataka Halmashauri ya Buchosa kuvitumia na kuvitunza viruri ili vilete tija kwa jamii.

Kwa upande wake Mkuu wa WIlaya ya Sengerma Mhe.Emmanuel Enock Kipole amesema heshima ambayo wamepewa na TCRA wataienzi kwa kutumia vizuri vifaa kituo hicho kwani kulingana na tekinolojia inavyokua vifaa hivyo vitapelekea kukua kwa uchumi wa Wilaya ya Sengerema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.