• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TEKNOLOJIA YA MRADI WA ZAIDI YA PAMBA USAMBAE NCHI NZIMA: WAZIRI BASHE

Posted on: March 28th, 2024

TEKNOLOJIA YA MRADI WA ZAIDI YA PAMBA USAMBAE NCHI NZIMA: WAZIRI BASHE


Mradi wa Zaidi ya Pamba (BEYOND COTTON) uliokuwa ukifadhiliwa na Serikali ya Brazil umefungwa rasmi leo mkoani Mwanza huku rai ikitolewa na mwakilishi wa Waziri wa Kilimo ambaye ni Mkurugenzi wa usalama wa chakula Gungu Mibavu kusambaza teknolojia iliyotumika kwa mikoa inayolima zao hilo.

Akizungumza na wanufaika wa mradi huo katika hafla ya ufungaji huo iliyofanyika shule ya Sekondari ya Janeth Magufuli kijiji cha Nguge wilayani Misungwi Mibavu amesema lengo la mradi huo uliotekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu ni kuleta tija kwa mkulima wa Pamba.

"Niwaombe taasisi zote za utafiti wa kilimo mlioshiriki mradi huu,muhakikishe utaalanu wote unawanufaisha wakulima wa Pamba kuanzia kuwa na mbegu bora,pembejeo na ulimaji wa kisasa,"amesisitiza kiongozi huyo mwandamizi kutoka wizara ya kilimo.

Amesema kumaliza kwa mradi huo kuwepo sasa na matokeo chanya kwa wilaya za Misungwi,Magu na Kwimba ambapo mradi huo uliotekelezwa na kuwa mfano kwa maeneo mengine nchini.

Balozi wa Brazili hapa nchini Mhe.Gustavo Martines amebainisha nchi yake ina miradi ya mazao mbalimbali ikiwemo sukari na kahawa hivyo wataendelea kushirikiana na Tanzania kadiri ya uhitaji utakavyoonekana.

"Mradi huu wa Zaidi ya Pamba umekwenda pamoja na utoaji wa elimu ya umwagiliaji maji na lishe hivyo nimefurahi kuona hapa kijiji cha Nguge namna mnavyotekeleza kwa vitendo,"Balozi Gustavo.

Tupo katika mpango mkakati kwa kushirikiana na wadau  kuanzia mwaka 2022 hadi 27 wa wa kutekeleza malengo ya kilimo kuanzia kuvuna hadi masoko,mradi huu wa Zaidi ya Pamba umekuwa sehemu ya mpango huo,"Sarah Gibson,Mkurugenzi mkazi Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula.

Awali katika mazungumzo mafupi na Balozi huyo mapema leo asubuhi Ofisini kwake, Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe.Amos Makalla amesema ana imani mwisho wa mradi huu ndiyo mipango ya miradi mingine zaidi ya kilimo hasa kutokana na Brazil kupiga hatua zaidi ya teknolojia katika sekta hiyo.

"Tunahitaji pia elimu zaidi ya kitaalamu ya kilimo cha Sukari tuna ardhi nzuri yenye rutuba,tunapungukiwa na utaalamu wa kuzalisha kwa tija",mkuu wa mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.