• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Tulilinde Ziwa Victoria ili litupe Matunda : Byabato

Posted on: September 26th, 2023

Tulilinde Ziwa Victoria ili litupe Matunda : Byabato


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Afrika  

Mashariki) Mhe. Steven Byabato leo Septemba 26, 2023 amefika Kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kufuatia ziara yake ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kisekta mkoani humo.

Akiongoza ujumbe alioongozana nao kwenye mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Byabato ametoa wito kwa wadau kwenye ukanda huo kulilinda Ziwa Victoria kwa maslahi ya vizazi vya sasa na baadae.

Amesema ziwa hilo linalounganisha Mataifa mbalimbali Afrika kwa dahari ya miaka limekua likistawisha uchumi wa Utalii na ukuaji wa sekta ya uvuvi hususani kwa nchi za Afrika Mashariki hivyo kila mmoja anapaswa kulilinda lisiharibiwe wala kuchafuliwa.

Tunalilinda ziwa letu ili nalo litulinde sisi, sheria za usimamizi wa bonde la ziwa Victoria ni lazima zizingatiwe ili ziwa letu lilete matunda kwetu sio tu kwa usafirishaji na chakula bali hata kwa uchumi wa uvuvi na Utalii." Amesema Byabato.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati Mkoani humo huku akitolea mfano wa Daraja la Kigongo Busisi, Meli ya MV Mwanza, Machinjio ya Kisasa, miradi ya usafi wa mazingira pamoja na mradi wa Maji wa Butimba ambao uko mbioni kukamilika.

Mhe. Makilagi amefafanua kuwa miradi hiyo ni kielelezo kwamba Mhe. Rais Samia amekusudia kuwahudumia wananchi kwa kuwaondolea kero kwenye huduma za kijamii kwenye sekta za Miundombinu,  Maji, Afya, Kilimo, Usafi wa Mazingira na Elimu.

Ziara ya Mhe. Byabato Mkoani Mwanza imejikita kwenye ukaguzi wa miradi mbalimbali ukiwemo Mradi wa Usafi wa Mazingira Pasiasi unaosimamiwa na Bonde la ziwa Victoria ambapo atajionea hatua ya utekelezaji iliyofikiwa kwenye miradi hiyo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.