• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TULINDENI NGUVU KAZI YA TAIFA KWA KUWACHANGIA FEDHA WATOTO WENYE SARATANI: RC MTANDA

Posted on: May 4th, 2024

TULINDENI NGUVU KAZI YA TAIFA KWA KUWACHANGIA FEDHA WATOTO WENYE SARATANI: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Mei 4, 2024 amezindua rasmi mbio za Bugando Health  Marathon zenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu kwa watoto wenye Saratani na wasio na uwezo wa kumudu matibabu hayo.

Akizungumza na washiriki wa mbio hizo kwenye Hospitali ya Bugando, Mtanda amezitaka Taasisi na wananchi wote watakaojaaliwa kuunga mkono zoezi hilo ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.

"Awali ya yote niupongeze uongozi wa Hospitali ya Bugando chini ya Mkurugenzi wake Dkt. Fabian Masaga, kwa ubunifu huu wa kutafuta fedha kwa nia njema ya kuokoa vizazi vyetu,ni ukweli gharama ya matibabu ya Saratani ipo juu na wengi hatuwezi kuimudu," Mhe.Mtanda.

Mkuu huyo wa Mkoa aliyeshiriki mbio za km 5 amesema mpango huo umekuja wakati mwafaka hasa kutokana na idadi ya watoto wanaogundulika na Saratani kuongezeka kutoka 50 kwa mwaka hadi 300, hivyo jitihada kama hizo zinapaswa kuungwa mkono.

"Nimeguswa na zoezi hili la uchangiaji na Ofisi yangu inatoa shs milioni 5 nikiwa na imani wengi mtajitokeza ili kufaniikisha malengo ya kuwasaidia watoto hawa,"amesisitiza Mhe.Mtanda

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando Dkt.Fabian Masaga amebainisha malengo ya mbio hizo za Marathon ni kupata zaidi ya shs bilioni moja zitakazowasaidia watoto wasio na uwezo,malengo mengine ni kuhamasisha jamii kujenga tabia ya kuchangia,kuhimiza kushiriki michezo na kufahamiana kwa ujumla.

"Ada ya ushiriki wa mbio hizi ni shs 35,000 na tutakuwa tukifanya mazoezi haya kila Jumanne na Ijumaa kabla ya kilele chake Agosti mwaka huu ambapo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dotto Biteko atakuwa mgeni rasmi,"Dkt.Masaga

"Ugonjwa huu unatibika endapo mtoto ataletwa mapema Hospitali,changamoto ipo kwa baadhi ya wazazi kuanza kukimbilia tiba mbadala na baadaye kuja Hospitali wakati tayari ugonjwa umepiga hatua kubwa,"Dkt.Yoronimo Kashaigili,bingwa wa ugonjwa wa Saratani kwa watoto.

Kauli mbiu ya mbio za Bugando Health Marathon inasema,Kimbia,changia watoto wenye Saratani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.