• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TULITUMIE JUKWAA LA UMISSETA NA UMITASHUMTA KUPATA HAZINA YA WANAMICHEZO WA TAIFA:RAS BALANDYA

Posted on: June 10th, 2024

TULITUMIE JUKWAA LA UMISSETA NA UMITASHUMTA KUPATA HAZINA YA WANAMICHEZO WA TAIFA:RAS BALANDYA


Mashindano ya Michezo ya Umoja wa Shule za Sekondari UMISSETA na Umoja wa Shule za Msingi UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Mwanza yamefungwa leo rasmi na rai kutolewa Jukwaa hilo litumike vizuri kupata hazina ya wanamichezo wa Taifa.

Akifunga mashindano hayo leo Alasiri kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Nsumba kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu Bw.Daniel Machunda amesema wanamichezo nyota wanaotamba hivi sasa Duniani wameanzia ngazi kama hizi na kupata muendelezo mzuri,hivyo hatuna budi kuvibaini vipaji vinavyoonekana na kuviwekea mkakati maalum wa kuviendeleza.

"Kwa muda mfupi nimekaa hapa nimeona uwezo mzuri wa vijana wetu hasa katika sanaa za ngoma na kwaya,ni jambo la kujivunia sana,hii ni hazina nzuri ya Taifa tunaishukuru Serikali kwa kuweka mashindano haya kila mwaka"amesisitiza Machunda.

Aidha amewataka wanamichezo wote bora waliopata nafasi ya uteuzi kwenda kushiriki mashindano ngazi ya Taifa kutanguliza nidhamu ambayo ndiyo silaha ya mafanikio.

"Sasa hivi wanamichezo ndiyo wanalipwa fedha nyingi Duniani,lakini hadi kufikia hatua hiyo nidhamu ndiyo silaha ya pekee ni lazima mjitambue,muwe wasikivu kwa walimu wenu,ongezeni bidii na kuzingatia maelekezo yote ya msingi huo ndiyo msingi wa kupata mafanikio,"Machunda

Akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Afisa Michezo Mkoa wa Mwanza,James William amebainisha mashindano hayo yameshirikisha michezo 9 ukiwemo soka kwa wavulana na wasichana,mpira wa kengele kwa albino na wenye ulemavu wa macho,mpira wa kikapu,pete,mezani,wavu na mikono kwa wasichana na wavulana pia imeshirikishwa sanaa za jukwaani ambazo ni kwaya,ngoma,mziki wa kizazi kipya(Singeli) na uchekeshaji.

"Ndugu mgeni rasmi tumepata jumla ya wanamichezo bora 120 na tumeongeza 40 tutafanya mchujo ili kuwapata 120 watakaokwenda kushiriki ngazi ya Taifa huko mkoani Tabora kuanzia Juni 17 hadi 27 mwaka huu",Afisa Michezo.


Katika mashindano ya ngazi ya Mkoa mwaka huu mshindi wa jumla ni Wilaya ya Nyamagana ikufuatiwa na jirani zao Ilemela.

Kwa miaka minne mfululizo Mkoa wa Mwanza umeshika nafasi ya pili Kitaifa kwenye Mashindano ya Umissseta

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.