• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TUMIENI PROGRAMU YA GPE AWAMU YA TATU KUBORESHA SEKTA YA ELIMU: RAS BALANDYA

Posted on: March 6th, 2024

TUMIENI PROGRAMU YA GPE AWAMU YA TATU KUBORESHA SEKTA YA ELIMU: RAS BALANDYA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amewataka wadau wa elimu kutumia programu ya kuboresha kada ya Ualimu (GPE) kuboresha mazingira ya ufundishaji ambayo ni pamoja na walimu kupata nyumba bora na vitendea kazi vya kufundishia.

Amezungumza hayo leo Machi 6, 2024 kwenye kikao kazi cha kutambulisha programu ya GPE awamu ya tatu kilichohusisha Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Elimu, Maafisa Mipango na wadau wa Elimu Mkoani Mwanza.

RAS Balandya amewaomba wadau wote kutumia muda vyema kuhakikisha wanaifahamu programu hiyo vizuri na kwenda kuitekeleza kwa ubora ili kusaidia kutimiza malengo yanayokusudiwa na program hiyo.

“Tutumie muda vizuri kujifunza kwa ukamilifu kuhakikisha program tunaifahamu vizuri na kwenda kuitekeleza kwa ukamilifu na kuwafikishia wote watakaohusika katika utekelezaji ili malengo yaliokusudiwa yatimie” RAS Balandya

Naye Afisa Mawasiliano Serikalini kutoka TAMISEMI, Fredrick Kibano amebainisha kwamba program hiyo inayolenga kuborehsa kada ya ualimu itaanza utekelezaji wake mara tu baada ya kuzinduliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan huku akibainisha kuwa Tanzania ilijiunga kwenye mradi huu mwaka 2013.


“Mradi huu umejenga shule za msingi mpya zaidi ya 14 ambazo zimepunguza uhaba na kutoa vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum, ujenzi wa mambweni kwenye baadhi ya mikoa, pamoja na nyumba za walimu ili kupunguza uhaba” Kibano.

Vilevile, wadau mbalimbali wameupongeza mfumo wa programu hii kwa kuweza kuleta mabadiliko kwa kuboresha Sekta ya Elimu hususani kwa kuwakumbuka waalimu kwa kuwajengea nyumba za kuishi ambayo ilikuwa ni changamoto kubwa kwa baadhi ya maeneo nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.