• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TUTUMIE MATAMASHA KUUTANGAZA UTAMADUNI WETU - DKT. BITEKO

Posted on: June 27th, 2024

TUTUMIE MATAMASHA KUUTANGAZA UTAMADUNI WETU - DKT. BITEKO


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dotto Biteko ametoa rai kwa Watanzania kutumia  matamasha makubwa kama la Bulabo (Tamasha la sherehe za mavuno) kutangaza mila na tamaduni za Mtanzania, ikiwa ni njia muhimu ya utambulisho wa Taifa la Tanzania kimataifa.

Mhe. Biteko ametoa rai hiyo alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Chifu Mkuu wa Machifu wote Tanzania (Chifu Hangaya) katika kilele cha Tamasha la Utamaduni la Bulabo Kanda ya Ziwa lililofanyika leo Juni 27, 2024 Bujora - Kisesa Wilayani Magu Mkoani Mwanza.

Mhe.Biteko amesema Taifa la Tanzania lina mila na tamaduni zake ambazo hurithishwa vizazi kwa vizazi ambapo ni lazima zilindwe na zihifadhiwe vizuri na kujiepusha na kupokea tamaduni za kigeni ambazo sio asili yetu.

"Ni lazima tulinde na kudumisha tamaduni zetu, Taifa lisilodumisha tamaduni zake, hilo ni Taifa la mazombi, hivyo ninawaasa tudumishe misingi ya mila, desturi na tamaduni zetu". Amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Aidha Dkt. Biteko ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Mwanza chini ya Mkuu wa Mkoa Mtanda kwa maandalizi mazuri na ya kiwango ya tamasha hilo la bulabo na kuahidi kwenda kuyasimulia hayo kwa Mh. Rais Samia, sambamba na hayo pia ametoa maagizo kwa Mikoa yote ya kanda ya ziwa kuhakikisha wanashirikiana vizuri katika kuandaa tamasha hilo kwa mwaka ujao ili kulifanya  kuwa la viwango.

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema wamedhamiria kulikuza na kuliendeleza tamasha hilo kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo na kulitangaza pia kimataifa ili nalo lifanywe kuwa ni kivutuo cha utalii kwa kanda ya ziwa.

"Nina hakika mwakani tamasha hili litakua bora zaidi na niwahakikishieni kuwa tutatarajia kupokea zaidi ya watalii 100 kutoka nchini Brazili watakaokuja kushiriki katika tamasha la bulabo, lengo ni kuutangaza utamaduni wa kabila la kisukuma kimataifa".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.