• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UKWEPAJI KULIPA KODI NI UKATILI UNALENGA KUUA UCHUMI WETU - RC MTANDA.

Posted on: February 20th, 2025

UKWEPAJI KULIPA KODI NI UKATILI UNALENGA KUUA UCHUMI WETU - RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa Viongozi wa Taasisi za Umma na zisizo za umma kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika kulipa kodi na kuhimiza watumishi walio chini yao kidai risiti wakati wote wanapofanya manunuzi ya bidhaa au huduma ili tujenge uchumi wa nchi.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo usiku wa leo Februari 19, 2025, alipokuwa akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mlipa kodi iliyofanyika katika Ukumbi wa Rock City Mall, Ilemela na kuupongeza uongozi mzima wa TRA kwa kuja na wazo hilo la namna ya kipekee kabisa la kuwashukuru walipakodi.

Aidha, Mhe. Mtanda ametoa rai kwa kila mmoja kuhakikisha analipa kodi sahihi na kwa hiari kwani kodi hizi ndio zinarudi tena kwetu katika mfumo wa huduma mbalimbali ambazo serikali inazitoa kwa wananchi wake.

“Sambamba na hilo niwakumbushe Mamlaka ya Mapato Tanzania kuendelea kutoa elimu ya kodi kwa wananchi ili kila mmoja aweze kutekeleza wajibu wake jinsi inavyompasa”.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda amewapongeza walipakodi wote waliopongezwa kwa kulipa kodi zao vyema na amewasihi zawadi hizo walizopewa kuwa chachu kwao na kwa wengine wengi kujifunza ya kwamba kodi ni jambo la kizalendo na linahitaji ushirikiano wa pamoja kati ya serikali na wananchi wake ili kuiwezesha nchi kupiga hatua zaidi na zaidi.

Naye Bw. Faustine Mdessa, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Mwanza, amesema ujio wa wazo hilo inadhihirisha kwamba TRA inathamini mchango

wa walipakodi katika makusanyo ya mapato ambayo yanaiwezesha serikali kutekeleza mambo mbalimbali yakiwemo kuboresha huduma za afya, ulinzi na usalama wa nchi.

Kadhalika amesema kuna kuna baadhi ya wafanyabiashara wanakosa uaminifu na kuwarubuni wateja kwa kuwashushia bei za bidhaa na huduma ili kuwapa risiti za bei ambazo sio sahihi hali inayopelekea mapato mengi kupotea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.