• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UTOAJI WA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHO SHULENI NI LAZIMA: RAS BALANDYA

Posted on: August 12th, 2024

UTOAJI WA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHO SHULENI NI LAZIMA: RAS BALANDYA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewataka wadau wa masuala ya Lishe Mkoani humo kuhakikisha chakula kinachopatikana kwenye shule za msingi na sekondari kinakua na virutubisho ili kutokomeza udumavu kwa watoto.

Ametoa wito huo mapema leo jumatatu ya Agosti 12, 2024 wakati akifungua Kikao kazi cha kujadili Afua za Lishe ambapo alibainisha kuwa suala la upatikanaji wa chakula kwenye shule za mkoani humo upo kwa asilimia 73 lakini ni asilimia 50 tu ndio kina virutubisho.

Bw. Balandya amefafanua kuwa kukosekana kwa chakula chenye virutubisho mathalani madini chuma na zinki pamoja na vitamini B 9 kumepelekea mkoa huo kuwa na udumavu kwa asilimia 27 kwa watoto walio chini ya miaka mitano kwa utafiti wa mwaka 2022.

Amesema, wasindikaji wanaochakata vyakula ili kupeleka kwenye shule za Mkoa huo ni lazima wahakikishe vinakua na virutubisho na kwenye hilo amewaomba Shirika la Viwango (TBS) kupitia ofisi ya Kanda ya ziwa kuhakikisha wanasaidia kudhibiti ubora wa virutubisho kwenye vyakula hivyo.

"Ubongo na akili ya mtoto hutegemea lishe bora anayopatiwa hivyo twendeni tukawape chakula chenye virutubisho shuleni na tutoe elimu kwa wazazi na walezi kupitia vikao vya shule kuhakikisha wanawapa chakula bora nyumbani ili uwezo waliojaliwa na Mungu uonekane" Amesisitiza Balandya.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba amesema ni vyema jamii ikajikita kwenye utoaji wa chakula chenye virutubisho ili kuwajengea watoto afya njema na kwa kufanya hivyo wtakingwa na tiba zitokanazo na udumavu au ukondefu ambavyo visipodhibitiwa jamii huingua kwenye kutibu maradhi.

"Afya bora ndio mtaji wetu wote, hatuwezi kufanya chochote bila kuwa na afya bora hivyo watoto wetu ni lazima wawe na lishe bora wakati wote ili tujenge Taifa lenye nguvu la sasa na la baadae." Ameongeza Mganga Mkuu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.