• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vifaa ujenzi wa Meli vyawasili

Posted on: July 20th, 2019


Agizo la Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kutoa siku nne kutaka  makontena yaliyo na vifaa vya ujenzi wa chelezo, ukarabati wa meli ya MV Viktoria na MV Bitiama  yaliyokwama Bandari ya Dar es Salaam kufika jijini Mwanza limetekelezwa ambapo jana makontena 10 kati ya 56 yalipokelewa Mwanza.


Makontena hayo yalipokelewa  na  viongozi mbalimbali wa Serikali akiwamo Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Elias Kwandikwa, Katibu Mkuu wizara hiyo-Uchukuzi, Mhandisi Leonard Chamriho, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella na Meneja wa Kampuni ya Huduma za Meli nchini ( MSCL), Erick Hamisi.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mapokezi hayo, Mhe.Kwandikwa alisema  anashukuru agizo la Mhe. Rais Dkt. Magufuli limetekelezwa ndani ya siku alizotoa  ambapo makontena yote 56 yameondoka jijini Dar es Salaam kulekea Mwanza na kati ya hayo 10 yamewasili salama.


“Sisi kama wizara tulipokea maelekezo na tumeyatekeleza kwa wakati, kilichobaki ni kuona kazi ya ujenzi wa chelezo na ukarabati wa meli ya MV  Viktoria  na MV Butiama inaanza haraka na kukamilika kwa wakati tena kabl aya Machi , 2020, zaidi ya yote tunashukurua kwa ushirikiano uliafanyika tangu agizo litolewa hadi leo napokea mizigo hii,”alisema Kwandikwa.


Naye Meneja wa MSCL, Hamis alisema  baada ya kupokea vifaa hivyo  atasimamia kwa ukaribu kazi hiyo na  itakwenda kwa haraka sana na kukamilika mapema huku akisisitiza hakutatokea kasoro katika ujenzi wa chelezo na ukarabati wa meli hizo.


Naye Mkuu wa Mkoa,Mhe.John Mongella alisema   sasa hivi hakutakuwapo na majadiliano kwani tayari Mhe.Rais Magufuli ametoa maelekezo ujenzi huo kukamilika kwa wakati, hivyo hataweza kumvumilia mtu yeyote anayetaka kukwamisha shughuli hiyo.


Julai 16, Mhe.Rais Dkt. Magufuli aliagiza Wandarasi wa wanaotekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa Meli mpya ya abiria na mizigo pamoja ukarabati wa meli za MV. Victoria, MV Serengeti na MV. Butiama kuhakikisha zinakamilika kwa wakati na kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.


Pia amemuagiza Msimamizi wa Mamlaka ya  Bandari ya Mwanza Kusini, Moris Mchindiyuza kuangalia maslahi ya vibarua wanaopakia na kupakua mizigo kwenye bandari hiyo ikiwa ni pamoja na kusajili majina yao ili waunde chama chao kusimamia masilahi yao.


 “Wahandisi na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano hakikisheni kazi hii inafanyika kwa ubora na umakini kwani haiwezekani Serikali ikatoa zaidi ya Sh. bilioni 152 kujenga meli na kukarabati nyingine halafu mradi unachelewe.











Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.