• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vijana 194 wahitimu Mafunzo ya Atamizi Mwanza,wapewa Rai ya kutanua wigo wa kujiajiri

Posted on: May 29th, 2023

*Vijana 194 wahitimu Mafunzo ya Atamizi Mwanza,watakiwa kutanua wigo wa kujiajiri


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewapongeza na kuwataka vijana walio hitimu mafunzo ya Atamizi kuziendeleza juhudi za serikali za kuongeza fursa ya ajira kwa vijana kwa kujiajiri na kuwaajiri wengine.

Mhe. Ulega ameyasema hayo leo Mei 29 wakati alipohudhuria hafla ya ufungaji mafunzo hayo ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji yaliyo chukua muda wa Miezi 3 ambayo imewakusanyisha wahitimu 194 wa awamu ya kwanza kutoka katika vituo 14 nchi nzima iliyofanyika Mkoani Mwanza katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Butimba.

"Nipende kuwapongeza vijana mnaohitimu  leo kwa hatua mliochukua ya kujifunza uvuvi kwa nia ya kuanzisha miradi ya uvuvi na ukuzaji wa viumbe maji inachangia kwa kiasi kikubwa kukuza juhudi za serikali za kukuza fursa za ajira  kwa vijana kupitia sekta ya uvuvi,"Amesema Mhe. Ulega.

"Kwa mwaka 2023/2024 wizara imepanga kuwawezesha vijana 750 kupata mafunzo kwa vitendo kwa vijana waliohitimu katika fani ya uvuvi na ukuzaji wa viumbe  maji nchini miongoni mwao watakua ni vijana waliopo katika mafunzo ya JKT."  Mhe. Ulega.

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Amos Makalla amesema sekta ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza uchumi wa Mkoa wa Mwanza.

"Sekta ya uvuvi ina mchango mkubwa katika kuinua uchumi kwenye Mkoa wa Mwanza shughuli ya uvuvi ni sehemu ya ajira kwa wananchi walio wengi kupitia biashara za samaki, kutengeneza vyombo vya kuvulia samaki na kwenye viwanda vya kuchakata Minofu ya samaki  hadi kufikia  Machi 2023  ambayo ni robo tatu ya mwaka wa fedha  2022/2023 zaidi ya Shilingi Bilioni moja zilikusanywa kutoka sekta ya uvuvi  zikiwa ni sawa na 31.125% ya makusanyo ya Mkoa",amesema Elikana.

Aidha, Bi. Happiness Meena, Naibu Katibu Mkuu Wizara  Mifugo na Uvuvi amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaongezea Vijana ujuzi kwa vitendo zaidi  ili waweze kuongeza ubunifu katika kile ambacho wamejifunza.

Vilevile, mwakilishi wa Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu  Kazi Vijana Ajira na wenye ulemavu Bi. Josephine Mwaijande amesema Ofisi yao ipo katika taratibu za  kujenga kituo kimoja cha kutoa mafunzo hayo katika mwali wa Katongo Mkoani Kigoma

Pia, Bi. Jovina Eliam ambaye ni mnufaika wa mafunzo hayo kutoka Dar es salaam  wakati akisoma Risala ameiomba serikali kuwapatia vitambulisho ambavyo vitawatambulisha kama wataalam na wabobezi wa maswala ya uvuvi na kuwatofautisha na wale ambao watakua hawajabobea katika mafunzo hayo

Lengo la mafunzo hayo ya ATAMIZI ambayo yamechukua ni kuwajenga vijana walio hitimu fani ya uvuvi  na ukuzaji wa viumbe maji ni kuondoa dhana ya kuajiriwa na hivyo kuweza kubuni miradi na kuanzisha kampuni hivyo kuchangia katika pato la Taifa na kutoa fursa za ajira kwa watanzania.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI

    May 21, 2025
  • MSINGI WA MALEZI BORA KWA MTOTO UNAJENGA TAIFA IMARA: RC MTANDA

    May 21, 2025
  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.