• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

VIJANA MWANZA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Posted on: March 29th, 2025

VIJANA MWANZA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI


Serikali Mkoani Mwanza imewataka Vijana wa Mkoa huo kuchangamkia fursa mbalimbali ili waweze kupata kipato kitakachowasaidia kujikwamua na umaskini pamoja na kuboresha hali ya maisha.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Machi 29, 2025 alipokuwa akizungumza na Vijana walioshiriki katika Kongamano la PPRA linalohusu Fursa za Kiuchumi Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema Serikali ya awamu ya sita imeweka mazingira mazuri ya kuimarisha vipato vya wananchi wote kupitia Mifuko ya Maendeleo kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu ambapo kwa sasa dirisha la mikopo limefungwa tangu Oktoba, 2024.

Aidha Mhe. Mtanda amesema Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023, imezitaka Taasisi zote za Serikali kutenga Asilimia Thelathini ya bajeti zake kwa ajili ya Makundi Maalum (Wanawake, Vijana, Wazee na Watu Wenye Ulemavu).

“Kiasi hiki ni kwa ajili ya Watanzania ambao wanaweza kujikusanya na kuunda vikundi rasmi vya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu, kisha washiriki kwenye tenda za Serikali”.

Ninawasihi sana, mfuatilie kwa makini taarifa mtakazopewa katika Kongamano hili, ili mfahamu jinsi ya kupata sehemu ya fedha hizi kupitia Mfumo wa NeST, na kujiinua kiuchumi. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Naye Mkurugenzi wa Generation Samia, ambaye pia ndiye mratibu wa kongamano hilo Bw. Omary Kimweri amesema wao kama Kizazi cha mfanikio au maarufu kama Generation Samia wamedhamiria kuyaunganisha makundi mbalimbali na fursa zinazotengenezwa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Ndugu Dennis Simba, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) amesema fedha hizo 30% Serikali ya Dkt. Samia sio fedha chache ni nyingi sana ambapo ni zaidi ya trilioni 5 kwa bajeti ya mwaka mzima

Kadhalika ameahidi kuendelea kutoa elimu ili makundi hayo yaweze kujipanga kwa kutafuta fursa mbalimbali na amesema mpaka leo ni takribani trilioni 15 zimekwisha tolewa tangu kuanza kwa sheria hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.