• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vitambulisho vya Machinga kutolewa kwa simu janja

Posted on: March 15th, 2021

Selikali mkoani Mwanza imesema ugawaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo (machinga) kwa mfumo wa kidijitali ni mkakati wa Rais John Magufuli, kuwapa nguvu wanyonge watoke kwenye  umasikini na hali duni za maisha.

Pia kutokana na zoezi hilo kuwa nyeti imeagiza Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huo kusimamia kwa weledi na umakini zoezi hilo ili kuwe na tija.

Agizo hilo liilitokea jana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela, wakati akizungumza na Wakuu hao wa Wilaya,Wakurugenzi wa halmashauri  na maofisa biashara kutoka wilaya saba za mkoa huo .

Alisema zoezi la kuwapa vitambulisho wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga, ni mkakati wa Rais Magufuli wa kuwapa nguvu za kiuchumi wananchi wanyonge na kuwafanya watoke kwenye hali duni ya umasikini na kupata hali bora zaidi.

Mongela alisema mfumo huo wa vitambulisho unalenga kujenga uwezo wa wananachi wetu, utambuzi wa matatizo ya wafanyabiashara hao na jinsi ya kuwasaidia kukuza uchumi wao  na uchumi wa mkoa na nchi kwa ujumla.

Alisema  zoezi hilo nyeti lilianzishwa na Rais Magufuli kwa makusudi kwa ajili ya kuwainua wanyonge kiuchumi hivyo ni vyema likakamilika mapema na kwa wakati ikizingatiwa Mwanza haijawahi kuchelewa.


"Mwanza tumepewa vitambulisho 84,000 hadi kufikia Julai,Mosi mwaka huu viwe vimewafikia walengwa wote, Mwanza hatujawahi kuchelewa kwenye zoezi hili hivyo wakuu wa wilaya, wakurugenzi na maofisa biashara nendeni mkasimamie kwa weledi na umakini jambo hilo nyeti liwe na tija, " alisema Mongela.


Alifafanua mgawo wa kila  halmashauri  za wilaya ambapo Wilaya ya Nyamagana na Jiji la Mwanza imepewa vitambulisho  23,000, Ilemela 20,500 , Ukerewe 5,500 huku Halmashauri za wilaya  za Buchosa, Sengerema,Magu, Misungwi na Kwimba zikipewa kila moja vitambulisho 7,000.


Kwa mujibu wa Mongela, mfumo uliowekwa mwaka huu, Mamlaka ya Mapato  Tanzania  (TRA), ndiyo watakaowajibika kuvigawa  vitambulisho hivyo vitakavyokuwa na pia pamoja  taarifa zote muhimu za kila mfanyabiashara mdogo atakayesajiliwa kwenye mfumo kama ilivyo kwa leseni za udereva .


Aidha kabla ya vitambulisho  hivyo kuanza kugawiwa maofisa biashara  na wataalamu  wa Tehama walizopata mafunzo wanalalamika kutoa elimu ya matumizi ya mfumo kwa watendaji wa mitaa, vijiji na kata ili waweze kuwahudumia kwa ufanisi wafanyabiashara  hao wadogo ambapo mwaka jana Mkoa wa Mwanza  ulipokea vitambulisho 88,000 vyenye thamani ya sh. bilioni 1.76.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.