• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

“ Wakuu wa Wilaya Nendeni Mkasimamie mapato ya Ndani”- Mongella

Posted on: August 2nd, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amewataka wakuu wapya wa wilaya za nyamagana na ilemela kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ili kuondoa aibu ya jiji la mwanza na manispaa ya ilemela kuwa miongoni mwa halmashauri nchini zilizofanya vibaya kwenye ukusanyaji wa mapato ya ndani katika mwaka wa fedha wa 2017/2018.

Mhe.Mongella ametoa agizo hilo wakati wa hafla ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya za Nyamagana,Ilemela,Magu na Ukerewe ambapo pia amewataka kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma katika halmashauri hizo.

Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya walioteuliwa ni Dkt, Severine Mathias Lalika (Ilemela), Mhe. Dkt Philis Mishack Nyimbi (Nyamagana), Mhe.Dkt.Philemon Sengati Lugumiliza (Magu) na Mhe. Cornel Lucas Boniphace Magembe (Ukerewe).

Aidha,Mhe.Mongella aliwakabidhi vitendea kazi ambavyo ni Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015, Sheria za serikali za mitaa (a) Mamlaka ya wilaya (Sura ya 287) na marekebisho yake(b)Mamlaka ya miji(Sura ya 288) na marekebisho yake, Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 na marekebisho yake, Mwongozo wa uwekezaji wa Mkoa wa Mwanza wa mwaka 2017,na  Masharti ya kazi ya Mkuu wa wilaya ya mwaka 2016.

“Fanyeni kazi kwa juhudi na ushirikiano kwa kusimamia utendaji kwenye Wilaya pia zingatieni ukusanyaji wa mapato na muwe wabunifu na kuacha mizaha kwa kupiga vita uvuvi haramu,komboeni majimbo na kuboresha mazao ya pamba,mpunga na harizeti,”alisema Mongella.


Awali aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe. Hadija R.R. Nyembo akitoa hotuba kwa wakuu wa Wilaya wanaoanza na kuwaasa kuwa  wasisite kuuliza pale penye utata pia wafanye kazi kama timu moja ili kuleta ufanisi na matokeo  mazuri kwa wananchi.

Kwa upande wao wakuu wa Wilaya  walioapishwa wamesema kuwa wanahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwa  viongozi waliostaafu  pamoja na wananchi na kuahidi kusimamia maendeleo ya uchumi na viwanda ili kuwainua wananchi kwa ujumla.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.