• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WA NGUDAMA - MISUNGWI WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA BARABARA

Posted on: September 13th, 2024

WANANCHI WA NGUDAMA - MISUNGWI WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA BARABARA


Wananchi wa kata ya Bulemeji na Idetemia Wilayani Misungwi wameishukuru Serikali inayongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 8 kwa kiwango cha changarawe pamoja na daraja vinavyogharimu zaidi ya Milioni 427.

Shukrani hizo za wananchi zimetolewa leo ijumaa septemba 13, 2024 kwenye ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa wakati akikagua mradi wa daraja linalounganisha vijiji vya Ngudama na Kaluluma linalojengwa kwa zaidi ya milioni 122 katika kijiji cha Ngudama.

Akiongea kwa niaba ya wananchi Diwani wa Kata ya Bulemeji Mhe. Rahma Emanuel amesema mradi huo umewapa heshima wananchi ambao awali walilazimika kulipa zaidi ya Shilingi elfu 7 kwa usafiri wa pikipiki kutokana na ubovu wa barabara lakini kwa sasa wanatumia Tshs. 2000 pekee.

Katika wakati mwingine Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 6, Matundu 10 ya vyoo na Ofisi ya Walimu kwenye Shule mpya ya Sekondari Mwasonge inayojengwa kwa zaidi ya milioni 121 kutoka serikali kuu (Sequip) na akaagiza ukamilishaji unaozingatia ubora.

Aidha, katika kituo cha mabasi cha Misungwi Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa ujenzi wa vyumba 20 vya maduka vilivyojengwa kwa zaidi ya milioni 79 kutoka fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo umebuniwa kwa ajili ya kusaidia kuongeza mapato ya Halmashauri kwa kupangisha na kwamba zaidi ya Milioni 8.5 zinatarajiwa kukusanywa kwa mwaka.


Kabla ya kuhitimisha ziara yake kwa kuwataka wananchi kutunza amani na kujiandaa kushiriki kilele cha Mwenge wa Uhuru 2024 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mhe. Mtanda amekagua jengo la Mionzi kwenye kituo cha Afya Misasi lenye thamani ya Milioni 68 na amewataka wananchi kutunza miundombinu hiyo ambayo pamoja na vifaa tiba vinagharimu milioni 302.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.