• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wataalam wa Afya watakiwa kutoa elimu ya chanjo

Posted on: October 17th, 2019


Wataalamu wa Afya Mkoani Mwanza wametakiwa kutoa elimu ya chanjo zinazotolewa chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya ili kuongeza hamasa kwa wananchi kupeleka watoto.

Agizo hilo limetolewa  mkoani hapa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. John Mongella wakati wa akizindua  chanjo ya rubella na surua kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

Alisema Wataalamu wote wa Afya waliopata mafunzo ya utoaji chanjo hiyo lazima pia wahakikishe wanatumia muda wao kutoa elimu ili kwa wale ambao bado hawana ufahamu wahamasike kupeleka watoto wao kupatiwa chanjo.

"Leo tupo hapa kuzindua rasmi zoezi la utoaji chanjo hii mkoani kwetu huku lengo letu kwa mwaka huu ni kuhakikisha tunafanikiwa kwa asilimia mia moja."

"Sote tunafahamu kuna wakati zoezi linashindwa kufanikiwa kwa kwa sababu kuna baadhi ya wananchi wetu bado hawana uelewa na wana mila potofu juu ya chanjo hii basi ni jukumu lenu wataalamu wa afya kuhakikisha mnatoa elimu kwa watu wote ili kuwaongezea chachu ya wao kuleta watoto wao kuchanjwa.

"Kwani mpaka sasa Maandalizi yameshakamilika na chanjo itaanza kutolewa leo hivyo ni wajibu wa kila Kiongozi toka ngazi ya mtaa  hadi wilaya kuhakikisha anasimamia zoezi hili ili lisije likaingia dosari kwa kuwa uwekezaji ni mkubwa sana.

"Mwisho niwakumbushe wananchi wote kama kauli mbiu inavyosema "Chanjo ni kinga kwa pamoja tuwakinge" kwa hiyo wote wazazi na wasio wazazi tuwajibike na tuifanyie kazi kauli mbiu hii ili tufikie malengo kama mkoa na Taifa kwa ujumla.

Awali akitoa taarifa fupi ya chanjo hiyo mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt.Thomas Lutachunzibwa  aliwataka wananchi kupeleka watoto kwa wingi kupata chanjo kwani imethibitishwa na shirika la Afya duniani WHO.


"Kwa mwaka huu matarajio ya mkoa ni kuwafikia jumla ya watoto zaidi ya laki tisa katika vituo 608 vilivyoandaliwa ambapo kwa chanjo ya rubella na surua lengo ni watoto 667 579  na polio ni watoto  266 140.

"Mara ya mwisho chanjo hii ilitolewa mwaka 2014 ambapo ufanisi ulikuwa ni asilimia 97 hivyo niwaombe wanaanchi kwa mwaka huu  tuwapeleke watoto kwa wingu wapatiwe chanjo ili ufanisi iwe mkubwa zaidi," alisema Dkt.Lutachunzibwa.

Kwa upande wake Katibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Mhe.Dkt. Zainabu Chaula amewataka wakazi wa Mwanza na Tanzania kuhakikisha wanaunga mkono chanjo hiyo.

"Chanjo hii ni moja ya juhudi za serikali kuhakikisha kuwa inafikia maadhimio ya kutokomeza kabisa magonjwa yasiyokuwa yakuambukizwa kwa watoto wadogo.

"Niwaombe wote kwa pamoja tuwapeleke watoto wetu wakapate chanjo kwani Serikali yetu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imefanya uwekezaji mkubwa ili kufikia malengo ya  Afya bora kitaifa,"alisema Dkt. Chaula.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.