• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watanzania wapewa Rai ya kuuenzi Muungano kwa kufanya kazi

Posted on: April 26th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  Mhe. Adam  Malima amewasihi Watanzania kuuenzi muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kutobaguana na kuuchukulia Muungano  kama nguzo ya mafanikio na kufanya kazi kwa bidii

Mhe. Malima amesema hayo leo Aprili 26 2023 katika Maadhimisho ya Miaka 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambayo ki mkoa  yamefanyika katika wilaya ya Kwimba na kuongoza uzinduzi wa zoezi la upandaji miti kwenye Chuo cha ufundi Veta ambapo Mkoa wa Mwanza umejipanga kupanda miti milioni 23

"Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umeleta mambo mengi ya kimaendeleo na waasisi wetu walituasa Muungano uende pamoja na kufanya kazi ili kulijenga Taifa letu," Amesema Mhe. Malima

Mbali ya zoezi hilo la upandaji miti,Mhe. Malima katika kutekeleza azma ya Muungano ni kazi ya kuijenga nchi,amezindua  mradi wa maji kwenye Kijiji cha Malembe kata ya Igongwa Wilayani Kwimba iliyogharimu zaidi ya Shs milioni 900  na kuwataka wananchi kuilinda miradi hiyo kwa faida ya vizazi vijavyo.

" Naishukuru Serikali hii ya awamu ya sita imeonesha kutujali wananchi wa Mwanza kwa kutupatia miradi ya kimkakati ambayo inachochea maendeleo katika mkoa wetu,". Amesema Mkuu huyo wa Mkoa

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu  Ludigija amesema wanajivunia na kuishukuru serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea fedha kwa ajili ya kuendeleza shughuli za  kijamii

" Wananchi wa Kwimba na maeneo ya jirani tunaishukuru na tunajivunia miundombinu na uwekezaji mkubwa ambao Rais wetu ameufanya kwenye Wilaya yetu ya Kwimba kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kijamii,". Amesema Mhe. Ludigija

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa ametumia maadhimisho hayo kuwaelimisha wazazi juu ya umuhimu wa chanjo na kuwahamasisha  kuwapeleka watoto kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kupata huduma hiyo.

" Nitoe rai kwa wazazi kuhakikisha watoto wote wanaostahili kupata chanjo wanapelekwa katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuhakikisha  wanajikinga na magonjwa,". Amesema Dkt. Rutachunzibwa

Tanzania huadhimisha Sherehe za Muungano kila ifikapo Aprili 26 huku Watanzania wakifanya shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa kama ishara ya kuuenzi Muungano huo uliofanywa na waasisi wetu Mwl Julius Nyerere na Abeid Karume Aprili 26,1964.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.