• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WATUMISHI WA MWANZA RS WATEMBELEA BWAWA LA UMEME LA MWL. NYERERE no

Posted on: February 21st, 2025

WATUMISHI WA MWANZA RS WATEMBELEA BWAWA LA UMEME LA MWL. NYERERE


Watumishi kutoka Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza wameanza ziara yao ya kwanza mkoani Pwani kutembelea Bwawa la Mwl. Nyerere lililopo eneo la Rufiji.

Watumishi hao wapatao 33 wakiwa njiani kuelekea Bwawani walipata fursa ya kuwaona baadhi ya wanyama wakiwemo Twiga, Tembo na Nyati kwenye eneo la hifadhi ya Taifa ya Nyerere National Park hali iliyochangia furaha ya kuona vivutio hivyo vya utalii.

Mara baada ya kuwasili eneo la mradi walipokelewa na mratibu wa mradi huo Mhandisi Fidelis Almasi na kutoa taarifa fupi ya mradi huo ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl Julius Nyerere miaka ya 70.

"Huu ni mradi mkubwa ambao umeigharimu Serikali Tshs Trilioni 6 na upo asilimia 96 unaotoa megawati 2115 na mashine zote 8 kati ya tisa zinafanya kazi,nadhani nyie ni mashahidi usumbufu wa umeme kukatika kama ilivyokuwa awali umepungua kwa asilimia kubwa",Mhandisi Almasi

Ameongeza kuwa mradi huo ni kitega uchumi cha uhakika kwa Taifa kwani umeme unaofuliwa hapo ni mwingi ambao nchi utaweza kuwauzia Mataifa ya jirani kama Kenya,Rwanda na Uganda.


Watumishi kutoka Ofisi ya mkuu wa mkoa walizidi kuhamasika na baadhi kupata na mshangao wa aina ya hali ya juu ya teknolojia iliyotumika kwenye mradi huo wakati walipotembezwa kuanzia kwenye chanzo cha maji yaliyochepushwa kutoka mto Rufiji na sehemu ya kufuliwa umeme huku asili ya mto huo ukibaki kama ulivyo bila kuharibiwa mazingira yake

"Nichukue fursa hii kuwapongeza kwanza kwa uzalendo wenu mlioutanguliza wa kufanya kazi kwenye mradi huu,ni dhahiri haya ni mazingira magumu kuwa mbali na familia zenu,hakuna eneo la shule jirani zaidi ya kuwepo kwenye mbuga ya Taifa,huu ni mfano wa kuigwa na sisi tutakuwa mabalozi wazuri wa kuyasema tuliyo yaona,"Janeth Sishila,Afisa Maendeleo ya Jamii

Kwa upande wake Mhasibu Mkuu kutoka Ofisi ya mkuu wa Mkoa Ndg. CP Abdul Bandamo amebainisha Serikali ya awamu ya sita inazidi kuleta mageuzi chanya ya kiuchumi mfano mzuri ni mradi huu,Rais Samia amekuwa akihimiza matumizi ya nishati safi na sahihi huu mradi utakuwa na tija kwa watanzania.

Mradi huo wenye mandhari ya kuvutia kuna eneo lipo kwenye mikoa ya Morogoro na Lindi.

Watumishi hao watahitimisha ziara yao Jumapili hii kwa kutembelea mradi wa Treni ya kisasa SGR Jijini Dar na baadaye asubuhi kupanda Treni hiyo hadi Jijini Dodoma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.