• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watumishi watakiwa kuzingatia sheria wakati wa maninuzi

Posted on: May 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa John Mongella, amewataka watumishi wa Umma mkoani humo kuzingatia misingi ya uadilifu na uzalendo wakati wanaopojishughulisha kwenye michakato ya ununuzi kwenye taasisi zao ili kuwezesha kupatikana kwa thamani ya fedha kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito huo wakati akifungua mafunzo ya Sheria, Kanuni, Miongozo na Mifumo ya Ununuzi wa Umma kwa watendaji na watumishi wa umma kutoka taasisi zilizopo mkoani humo. Mafunzo hayo yana lengo la kuwajengea uwezo watumishi hao katika kutekeleza majukumu yao ya Ununuzi kwenye taasisi zao kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Ununuzi wa Umma.

Mhe. Mongella amesema maendeleo ya Halmashauri za mkoa huo yanategemea sana ufanisi wa watumishi hao katika kutekeleza shughuli za Ununuzi  kwa kufuata Sheria na Kanuni za Ununuzi wa Umma ambazo, pamoja na mambo mengine, zinataka wadau wote wanaohusika kwenye michakato ya ununuzi kuzingatia misingi ya uadilifu na uzalendo.

Lazima tuzingatie misingi ya uadilifu na uzalendo kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu na kuunga mkono azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Niseme tu kwamba hata kwenye Mkoa wa Mwanza, ikithibitika ukosefu wa uadilifu na uzembe wa wazi kabisa kwa watumishi wetu lazima hatua kali zichukuliwe dhidi yao, alisema Mhe. Mongella.

Aidha, Mhe. Mongella alimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kuwa taasisi zote za umma zilizomo mkoani humo zinafanya ununuzi wote kwa kuzingatia na kutumia Mfumo wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya kielektoniki (TANePS) ili kutekeleza matakwa ya Sheria pamoja na maagizo ya Serikali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kujenga Uwezo na Huduma za Ushauri wa PPRA, Mhandisi Mary Swai, alisema kupitia mafunzo hayo washiriki watafundishwa kuhusu matumizi sahihi ya utaratibu wa force account ambao taasisi nyingi za umma huutumia sana wakati huu.

Tunafahamu kwamba utaratibu wa Force Account umekuwa na changamoto kadhaa katika utekelezaji wake, ingawa njia hii ilianza kutumika kwa lengo zuri la kupunguza gharama. Baadhi ya changamoto ni usimamizi hafifu wa miradi unaotokana na wasimamizi kukosa ujuzi wa masuala ya ujenzi. Pia, kutowezeshwa gharama za usimamizi pamoja na kukosa uadilifu kwa baadhi ya wasimamizi, alisema Mhandisi Swai.

Mafunzo hayo ya siku tatu yamehudhuriwa na takribani washiriki 100 wakiwemo Wajumbe wa Bodi za Zabuni, Wakuu wa Idara Tumizi (user departments, watumishi kutoka vitengo vya Usimamizi wa ununuzi, Wanasheria, na Wakaguzi wa Ndani kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza na taasisi mbalimbali za mkoa huo.  

PPRA imeshaendesha mafunzo kama haya kwenye mikoa 15 nchini, Ruvuma, Njombe, Iringa, Kagera, Shinyanga, Kigoma, Geita, Rukwa, Katavi, Tabora, Mbeya, Dodoma, Songwe, Mara na Simiyu, ambapo huu wa Mwanza ni wa 16.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.